Tuesday, August 30, 2011

Na Aisha Mbaga

Mpenzi msomaji wa safu hii nakukaribisha tena uungane nami katika chumba changu hiki cha mahaba tuweze kujimwayamwaya na kujinafasi kwa raha zetu.Wiki uliyopita tulikuwa tukizungunzia udhaifu wa wanaume katika suaka zima la mapenzi na sababu zinazopelekea wao kuwa katika hali hiyo.tilibaini kuwa kwa upande mwingine wanakuwa na usongo wa kutimiza lengo hivyo wanapofika katika mchezo wakajikuta wameshindwa kuukwea mnazi, upande mwingine ni maumbile ya kibaiolojia na upande mwingine wanawale tunachangia kwa kutokuwa makini ama kujihusisha na mapenzi kwa wakati.leo nataka kuueleza jinsi wanawake walivyo wezi wa mabwana wa mashoga zao na jinsi wanavyoweza kusambaratisa penzi lililoota mizizi.
mwanamke anapotaka kukufanyia unyama kwa mpenzio hashindwi haswa pale unapokuwa umemweka karibu na mpenzio.kila mwanamke huwa na shoga na wengine hupenda kusema mambo ya kweli wanayoyapenda wapenzi wao na kumpa nafasi kubwa rafiki yake pale anapotaka kuporomosha penzi hilo.mwanamke anamitego mingi kwa mwanaume ikia i pamoja na kumpelekea zawadi ambazo mpenzi wake hampi.kumfanyia mambo ya mahaba ambayo hayapati kwa mpenzi wake na kisha kumtega kwa vivazi, na urembo wa asili. kina mavazi ambayo yamnamvutia mwanaume apende asipende, atatamani kuwa na wewe, mavazi haya si lazima yawe mini sket au top na pedo, waweza vaa hata baibui lakii kutokana na jinsi lilivyo likamvutia mwanaume na kujikuta anashindwa kujizuia na kuingia katika mtego wa mhaba mazito ambayo anadhani kuwa atayapatantoka kwako. kinachosababisha matatizo haya ni kutokana na kuaminiana kwa hali ya juu kati ya mashoga hawa na kuambiana siri zao za ndani juu ya wapenzi wao. ukweli ni kwamba, usipende kumweleza rafii yako mambo ya anayokufanyia mpenzio kwani unampa nafasi ya kuweza kumteka hususani anapojua kuwa mpenzio anaudhaifu gani. kama kunaulazima wa kuhadithiana juu ya wapenzi wenu, kuwa makini na wakati mwingine ni heri umwambia rafukiyo uongo ili kuweza kulinda penzi kwani kikulacho kinguoni kwako. wanawake wengi hawapendi kuona mwenzao kafanikiwa, ama kuona penzi la mtu likiwa imara, ni dhahiri kuwa wapo wanaochukia na kutafuta mbinu za kuliporomosha hata wakishindwa wao watatumia watu wa pembeni yenu bila ya wewe kujua kuwa shoga, rafikiyo mkubwa anakugeuka na kukuzunguka. waweza kusema sitaki kuwa na rafiki mwanamke kutokana na tabia za baadhi yao kuwa za unafiki na wivu kwa maendeleo ya mtu. kama ujuavyo mapenzi ni makubaliano kati ya watu wawili na yanaweza kuvunika muda wowote endapo wanaweza kushindana na kutofikia malengo. hilo si jambo la ajabu kwani ndio maana hata leo tunaweza kuona kwenye baadhi ya michezo ya tamthilia watu wakiamua kutalikiana ili kila mtu aishi kwa amani. ni mara chache sana waweza kumuona mwanake anasikitika kwa kuona penzi la mtu likiishia mitini hususan pale watu hawa wanapokuwa wachumba ama ndio kwanza wanaanza, achilia mbali waliooana na kuchokana. wanawake wengi wako makini kuhakikisha kuwa ndoa ya mtu fulani haifungwi na kufanikiwa kuvunja uchumba wa wawili hawa na wakati mwingine ndo kwanza maapenzi yanaanza lakini yataingiliwa na kidudu mtu na kuharibiwa. yote haya ni kutokana na mashoga na chanzo ni kupeana siri za wachumba wenu. tuweni makini na tuache kuaminiana kwani umwaminiye ndiye adui yako.

napenda kuwashukuru wasomaji wangu walionipigia simu na kunipongeza na pia kunipa ushauri, nakarubisha maoni yenu kwangu na nitayafanyia kazi bila kusita. pia napenda kumpa pole mama yangu ambaye aliniambia kuwa mumewe amekuwa kicheche kwa kutembea na watoto wadogo anaoweza kuwazaa bila kujali walipotoka na uzee walionao. napenda kumshauri mama huyu kutoka Tabata jijini Dar es Salaam kuwa asijali kuona mumee kamsaliti kwani hiyo ni kawaida ya wanaume wengi ila lamsingi namshauri amwombe wakapime afya zao kulingana na hali tuliyonayo.

kwa maoni na ushauri wasiliana nami kwa simu namba 0755-690690.

No comments:

Post a Comment