Tuesday, August 30, 2011

Hatimae leo tumeshuhudia Japani ikiungana na timu kama engalnd, marekani na nyinginezo katika kuyaaga mashindano ya kombe la dunia
Pamoja na japani kutolewa katika mashindano hayo lakini mejitahidi mpaka tone la mwsho lakini bahati haikuwa yao.  katika huu mzunguko wa robo fainali ya kombe la dunia mechi hii ndio naiona kama imekuwa kinyumea na matarijio ya wengi kwani kila mtu aliamini kabisa kuwa japani ndio timu yenye kiwango kikubwa cha mpira kuliko Paraguay hivyo kumfanya kila mtu kusema kuwa Paraguay hawachuki raund lakiniimekuwa sivyo.
Japani ambayo hata katika viwango vya shirikisho la mpira wa miguu duniani (FIFA) inashika nafasi nzuri kabi huku ikiwa ni ni tuimu iliyokuwa ikiaminika kama ni miongoni mwa timu bora kabisa  kati ya timu zinazoshiriki michuano ya kombe la dunia lakini cha kushangaza leo inapelekwa pelekwa na Paraguay kama vile watoto wadogo yaani wamebanwa kila kona na kushindwa kuonesha manjonjo yeyote ambapo mpaka kipndi cha mapumziko paraguiay walikuwa wakiongoza kwa ball position.
Japani ambao waliingia kwa kasi ya ajabu katika kipindi cha pili lakini walishindwa kufikia lengo kutokana na kukuta bado Paraguay wamekaza kama mwanzo, pia Japan walipata fursa nyingi lakini washambuliaji wao walikuwa wataitiwa ile mbaya hivyo kuifanya timu nzima ya japa kuonekana hakuna ktu.
Japani ilifanya mabadliko ya kumtoa Yukiabe na kumuingiza Mukabere dakika ya 80 lakini haikusaidia kitu kwa Paraguay ilikaza mpaka dakika ya mwisho hivy kuongezewa dakika 30 tena za kupambana na katika daklika ya 15 katika zile dakika30 za za nyongea japani ilifanya mabadiliko mengine ya kumtoa Okubo na kumuingiza Tamada ili kuongeza mashambulizi lakini bado hali ilkuwa ngumu. Mpaka kufikia dakika ya mwisho mechi ilikuwa ni dro ikiwa hakuna timu iliyoweza kuona lango la mwenzake hivyo kufanya refa awape penalt.
Dakika zote 30 zilikuwa ngumu kila upande kwa kutofungana na kasha kupeawa panalt tano tano. Katika panalt hizo hapo ndipo japani walipoona joto ya jiwe kwa kupigwa mikwaju yote mitano huku yenyewe ikikosa mkwaju mmoja nakuifanya ifungashe virgo na kurudi kwao japani huku wakiacha mashindano yakiendelea. Tusubiri mechi ya pili tuone nani ataibuka mshindi kati ya Hispania na Ureno ambae atakuja kucheza na Paraguay.

No comments:

Post a Comment