Tuesday, August 30, 2011

Kwanini wanaume hufika kileleni mapema
By Aisha Mbaga.

Hiyo ni kutokana na kushindwa kujidhibiti wakati wa mechi hadi pale wote wawili mtakapokuwa mtakaribia kufunga goli muweze kufunga pamoja.

Kufika kileleni mapema ni tatizo linalowakabili wanaume wengi wakati wa mapenzi. Mara nyingi tatizo hili hutokea katika siku ya kwanza kabisa mwanaume akutanapo na mwanamke ampendaye au anayeanzisha uhusiano nae kwa mara ya kwnza kukutana ni jambo la kawaida kwa mwanaume kushindwa kujimudu na kujikuta kafunga goli wakati mwenzake ndo kwanza anawasha moto.

Mwanaume anapomsotea mwanamke kwa muda mrefu, siku akimpata basi ni lazima mwanaume huyo kujikuta anashindwa kuucheza mchezo kiufundi na kujikuta kapanda mnazi na kuzdondosha zake kabala mwenzi wake hajafika popote.

Hata hivyo kua katika hali hii si ugonjwa bali ni hali ya kawaida tu ingawaje humfanya mmoja wenu kutofurahia na kujikuta akiwa na hamu ya kuendelea huku mwingine kachoka.pia kibaiolojia, tatizo hili linasababishwa na ukosefu wa uwiano wa “Homon” ikiwa homona zenu hazija zoeana, mwanaume anaweza kuona kuwa mwanamke hana ladha ile anayoitaka.

Sababu hiyo inaweza kumsababisha mwanaume kuvuta hisia kwa kumkimbuka mwanamke ambaye humfikisha na kumpa ladha anayoitaka ili aweze kukamilisha tendon a mwanake aliyenaye ka wakati huo hivyo anaweza akajikuta akilitaja jina la mwanamke mwingine wakati yuko na mwanamke mwingine.

Kisaikolojia hali ya kufika kileleni mapema bila mpangilio inasababisha na kushindwa kujiamini kwa mwanaume. Hapa ni kwa yule mwanaume aliyemsotea mwanamke kiasi cha kufikia hatua ya kukaribia kukata tama na baadae kujikuta kafanikiwa.

Mwanaume huyo huwa na kimuhemuhe cha kumpanda mwanamke huyo hivyo kujikuta kuwa amuonapo tu mrembo wake yeye anakuwa hahitaji tena maandalizi na ukimchekeweshea anaharibu mambo kabla ya kuanza kulili tunda lenyewe.

Kutokana na kutojiamini kwake, mwanuame huyo atakuwa akiwaza kama ni kweli ama ni ndoto kuwa na kimwana kama huyo aliye masotea kwa muda mrefuna sasa amefanikiwa kumuweka katika mikono yake, lazima mwanaume huyu atachetuka avuliwapo nguo na mwanadada huyu.

Kwa kawaida wanaume wengi hupenda wafanye mapenzi kwa dakika nyingi zaidi ili mwawa firahishe wapenzi wao lakini bila ya kutarajia wanajikuta wakiwa wamezidiwa nguvu na vimwana wao na hiyo ni kutokana na kuwa haijalishi kuwa ni muda gani maalumu wa mwanaume anatakiwa awe anafanya mapenzi kabla ya kufika kileleni.

Hebu tujiulize kwamba kuna ambaye anaweza kujizuia kufika kileleni mapema? Jibu ni kwamba unaweza ila cha msingi ni kuwa mtulivu na kuondfokana na wasiwasi, yaani unapaswa kujiamini kuwa unawza na umeshinda kuwa na huyo.

Usifanye mapenzi kwa kukomoa na wala usipanie sana kuwa lazima nikikutana na e niingie, jiamini kuwa ni wako na muda wote uko naye na unaweza kuchezanae upendavyo kwa kutumia muda wako.

Nimuhimu kujitambua kuwa utafika kileleni kwa wakati gani hivyo unaweza kujizuiakatika hatua hii muhimu kwa kujifunza na kuzoea.

Basi mpenzi msomaji wa safu hii napenda kukuaga kwa leo ila nakusihi tujumuike soto katika safu hii toleo lijalo.

No comments:

Post a Comment