Tuesday, August 30, 2011


SI MAKOSA YETU NI MAKOSA YENU KUTUTENGANISHA.

Hayo ni maneno yaliyozungumzwa na wanandugu wa baba na mama mmoja. Inakuwa vigumu na anaendelea kuniwia vigumu kuvumilia kisa cha dada na kaka kuishi pamoja kama mke na mume na kuzaa watoto.
Ni familia moja ya kitajiri ambayo wazazi wao walitengana na kugawna watoto.
baba alichukua mtoto wa kiume na mama akamchukua binti yake.
Katika makuzi ya watoto hao hawawahi kujuana kuwa ni ndugu kutokana na kila mmoja wao kulelewa na mzazi mmoja na kufichwa juu ya mwenzie. usemi wa hakuna siri duniani unasimama pale wanandugu hao wanapokutana na damu zao kuvutana kiasi cha kila mmoja kuwa na hisia za kimapenzi kwa mwenzie.
Hawakuficha hisia zao, kila mmoja aliweka bayana ajisikiavyo kwa mwenziwake. mwisho wa yote waliamua kuishi kama mtu na mpenziwake na wakazaa watoto wanne.
mtihani unakuja pale ambapo wanagundua kuwa ni damu moja na jamii kuwataka watengane. hilo limekuwa gumu na kwao halitowezekana kwani kwa sasa wanafanya taratibu za kufunga ndoa. wao wenyewe wanasema wanapendana na hawawezi kuachana.
kama ni makosa wao kukutana na kuwa wapenzi ni ya wazazi wao na si kosa lao kwa ni endapo wazazi wao wangewakutanisha mapema wasinge fikia hapo walipo kwa sasa. wazazi wa watoto hao walijengeana chuki na kila mmoja kummiliki mtoto mmoja kama mali yeke na hakuna ambaye alitaka kumpeleka mtoto aliye naye kwa mzazi ambaye yuko mbali naye.
matatizo hayo hutokea mara nyingi pale familia zinapokorogana.
lamsingi ni kwamba wanandoa wanaposhindwana , wasiwatenganishe watoto ili kukwepa majanga kama hayo ya mtu na dadake wa kuzaliwa tena baba na mama mmoja wanaishi kama mke na mume na tayari wanawatoto na wameapa kila mmoja wao kuwa hawataachana labda kifo kiwatenganishe kama maandiko matakatifu yasemavyo.
Ndivyo Dunia ilivyo hivyoo.
UHUMI WA TANZANIA UTABOREKA TU



Na Aisha Mbaga
RAIS wa Jamuhuri ya Muungano Tanzania, Jakaya Kikwete, amesema serikali ya awamu ya nne itaendelea kuamini kuwa, sekta binafsi ni moyo wa uchumi na maendeleo ya Watanzania na Taifa kwa ujumla.
Kikwete alisema kuwa, Serikali, imeweka mazingira mazuri katika kuhakikisha kuwa, fursa zote zilizopo kwenye uwekezaji, zinatumika kikamilifu kwa manufaa ya Taifa.
Hali kadhalika, alieleza kwamba, amewataka wawekezaji wa nje na ndani, kujenga imani na serikali yake ambayo alisema itafanya kazi na wadau hao kwa faida ya pande zote.
Katika Mkutano wa sita ulioandaliwa na Baraza la Taifa la Biashara(TNBC) uliofanyika mjini arusha, aliwataka wawekezaji kuwa na imani na Tanzania kwani ni nchi ambayo inaamani na inayopiga hatua kimaendeleo.
Lengo la mkutano huo ilikuwa n i kujadili masuala muhimu ya kiuchumi yatakayoiwezesha Tanzania kuondokana na mfumo wa uchumi hodhi.
Rais Kikwete ambaye pia ni Mwenyekiti wa TNBC, alisema kwa kuthamini mchango unaotolewa na wawekezaji wa ndani na nje, serikali yake imekuwa ikifanya mabadiliko katika baadhi ya sheria za biashara, zilizoonekana kukwamisha mikakati ya kuwezesha wawekezaji wa nje kuja nchini kuwekeza, hususan wa sekta za viwanda, madini na kilimo.
Alitaja baadhi ya sheria ambazo zimekuwa changamoto kwa wawekezaji wa ndani na nje zilizofanyiwa marekebisho kuwa ni ya ardhi na sheria ya kazi ambayo wawekezaji wengi ama waajiri wengi, wamekuwa wakidai kwamba, zinawakandamiza mno waajiri na kuwapendelea zaidi waajiriwa.
Alisema Kikwete Kuwa, "Kwa kuthamini mchango wa wawekezaji ambao wamekuwa wakisaidia maendeleo ya taifa, hususani katika suala la mapato ya serikali kutokana na biashara wanazoziendesha, serikali imekuwa ikijiendesha kutokana na kodi zinazotozwa toka kwenye sekta binafsi",.
Alisema, tayari Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeaanza kuangalia sheria hizo.
Alitaja hatua nyingine ambayo serikali ipo kwenye mchakato wa kuifanyia marekebisho kuwa ni ya vibali na leseni za biashara hapa nchini, hususan kwa wawekezaji wa nje.
Alisema kupitia mkutano uliopita wa Baraza la Taifa la Wafanyabiashara, wawekezaji wa nje walieleza kwamba changamoto kubwa wanayokumbana nayo ni vibali vya kufanyia biashara kuwa vya bei ghali ikiwa ni pamoja na urasimu wa kuvipata.
Rais Kikwete alisema, tayari ameziagiza mamlaka husika, kuangalia upya suala hilo ambapo alieleza kwamba, kiwango cha kulipia vibali vya kufanya biashara hapa nchini kitapunguzwa kuliko ilivyokuwa hapo awali.
Aidha alisema, "azma ya serikali kwa kushirikiana na baraza hilo ni kuhakikisha sekta binafsi zinapewa nafasi ya kuongoza ujenzi wa uchumi wa nchi, huku serikali ikiwa na kazi moja ya kujenga mazingira bora zaidi ya ufanyaji biashara".
"Natumaini kupitia mkutano huu, kasi dhidi ya ukuaji wa uchumi wa Taifa letu itaongezeka maradufu kupitia sekta binafsi zitakazowekeza hapa nchini, hasa kwa upande wa elimu, kilimo, utalii, viwanda, miundombinu, mawasiliano na sekta ya madini", alisema Rais Kikwete.
Hata hivyo, aliwataka wawekezaji kushirikiana na serikali katika kuboresha miundombinu, hususan ya barabara, ambapo alisema wawekezaji nao ni muhimu wakachangia ujenzi wa barabara badala ya suala hilo kuachiwa serikali pekee.
Kutokana na mabadiliko ya utandawazi pamoja na kuongezeka kwa gharama za kuendeshea sekta ya utalii, Rais alisema kuwa serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii ipo kwenye mpango wa kuongeza kodi ya watalii wanaoingia nchini kila mwaka kwa ajili ya kutembelea mbuga za wanyama.
Alisema gharama zimekuwa ni ghali mno kuliko awali hasa suala la kuboresha miundombinu ya barabara katika maeneo ya hifadhi za Taifa pamoja na barabara zinazokwenda kwenye hifadhi hizo.
"Serikali iko kwenye mchakato wa kuongeza kodi za watalii wanaoingia, ili kuboresha huduma ya utalii na kuongeza pato la Taifa", alisema JK.
Kuhusu suala la sekta ya kilimo, Rais Kikwete alisema kwa kuthamini kilimo ambacho ndicho uti wa mgongo wa taifa, kwa sasa serikali inaandaa mpango ya kuboresha sekta hiyo kwa njia ya kilimo cha umwagiliaji na utumiaji wa mbolea ili kuleta tija zaidi.
"Katika sekta ya kilimo, bado tunazidi kujitangaza ili kuzidi kuwavutia wawezekaji, kwani sekta hii ndio kitega uchumi cha Watanzania wengi na tegemeo kubwa kwa taifa letu", alisema Kikwete.
Alisema, kwa sasa kilimo cha umwagiliaji ndicho kinachopewa kipaumbele, ambapo aliwataka wawekezaji wa sekta ya kilimo kuja nchini kwa ajili ya kuwekeza hasa ikizingatiwa kwamba Tanzania ina vyanzo vingi vya maji kama mabwawa, mito, mifereji ambayo inafaa kwa kilimo cha umwagiliaji.
mapenzi ni nguzo ya kujenga familia

Na Aisha Mbaga

Mengi yameongelewa na yatazidi kuongelewa kuhusiana na hali halisi katika uwanja wa mapenzi.

Mimi nazungumzia hali hiyo lakini katika upande wa kuanzisha , kuboresha na kuyalinda mapenzi ya dhati.

Nimekusudia kukutandikia uwamja huu kwa sababu mapenzi ni kitu kisichokwepeka.

Hakuna binadamu anayeweza kukyakwepa mapenzi, kukwepa kupenda ama kupendwa kutokana na kuwa hayo ni maumbile.

Kwa kawaida mtu umpendae kuwa hukosi hamu ya kuonana naye kama ilivyo kwa mama na mwana ama mwana na mama ila katika mapenzi ya msichana na mvulana mambo hubadilika na kuwa ya ndani zaid.

Ukiwa na hamu ha hali ya juu kwa mpenzio basi upo katika kilele cha mapenzi na hutakiwi kushuka kwani ukiona unashuka kiwango cha kumuona mpenzio basi ujue kunahatari ya kusambaratika kwa mapenzu yenu.

Napenda kuanzia kukiandaa chumba cha mapenzi, ama uwanja wa mapenzi. Si lazima iwe kitandani tu, waweza badili uwanja kwa kuhamia bafuni ama kochini nap engine gaeini.

Kwanza kisafishe chumba chako vizuri kwa kifita vumbi kila kona .

Hakikisha kuwa unakipamba chumba chako kwa mauwa na kadi kama unazo.

Kifukize chumba chako udi ili kukifanya kinykie vizuri ama kipulizie marashi ya sluud kama unauwezo nayo, kama huna waweza tumia hata air freshna.

Kinachotakiwa ni kuiandaa sehemu yenyewe. Kama kitandani, tandika kitanda chako vizuri kwa shuka lemuye mauwa ya kuvutia, kama ni jeupe na halina mauwa, waweza kuchukua mauwa ya asumini ukayamwaga kitandani bna kuyatandaza vizuri. Ukikosa asumini waweza tumia mauwa ridi,. Mauwa haya huwa yanaharufu nzuri.

Waweza yatandaza nyumba nzima kama waweza ama chumba kizima kiwe kinanukia asumini,

Baada ya hapo hakikisha kuwa unausafisha mwili wako vizuri na kuuweka safi kwa ajili ya kuingia uwanjani kucheza mechi ya mahaba.

Fahamu kuwa kunamaks ambazo unaweza kuzipata ukiwa uwanjani ama ukazikosa hivyo ili kujiweka katika kiwango cha juu cha ufundi wa kufunga magoli ya mapenzi, ni lazima uwe na juhudi, usichoke na uwe makini katika mchezo ili uhakikishe mnatoka sare kwa kufunga goli.

Kwa kufanya hivyo utakuwa umefaulu mechi yako na utajiweka katika nafasi ya juu kiasi cha kumfanya mpenzio kukukumbuka kila awapo.

Sasa nakupeleka katika kuuandaa mwili wako.

Nenda bafuni uoge vizuri na ujisafishe sehemu zako zote nyeti za mili vizuri kwa kuuweka mili wako safi ili mpenzio aweze kuutembelea apendavyo.

Jitie manukato laini. Jifukize ikili yako udi na hakikisha kuwa wakati wa kujifukiza unamimina marashi ya aluud ili kuiruhusu harufu nzuri kupenya sehemu zote.

Fukiza nyele zako na nguo zako utakazovaa kabla ya kuingia uwanjani.

Andaa kitezo chako na moto kisha kiweke udi na uendelee kupendezesha chumba chako.

Andaa kitambaa cha pamba, mji ya mojo kwenye chupa na kibeseni kwa ajili ya kujisafisha mara baada ya mechi wewe na mpenzio.

Aingiapo mpenzio tia marashi ya aluud kwenye kitezo kisha mkaribishe uwanjani na muanze na mazoezi kabla ya mechi kali.

Wakati mnaendelea na mechi udi na marashi ya aluud yanapenya kwenye miili yenu taratibu na kuburudisha.

Kumbuka kutumia kitambaa chako laini kujisafishia taka zote baada ya mechi kali kisha nendeni wote bafuni mkaoge. Ikiwezekana endeleeni kujipa raha humohumo bafuni.

Ka leo tuishie hapo ila nakusihi usikose kujiunga nami toleo lijalo.
Kwanini wanaume hufika kileleni mapema
By Aisha Mbaga.

Hiyo ni kutokana na kushindwa kujidhibiti wakati wa mechi hadi pale wote wawili mtakapokuwa mtakaribia kufunga goli muweze kufunga pamoja.

Kufika kileleni mapema ni tatizo linalowakabili wanaume wengi wakati wa mapenzi. Mara nyingi tatizo hili hutokea katika siku ya kwanza kabisa mwanaume akutanapo na mwanamke ampendaye au anayeanzisha uhusiano nae kwa mara ya kwnza kukutana ni jambo la kawaida kwa mwanaume kushindwa kujimudu na kujikuta kafunga goli wakati mwenzake ndo kwanza anawasha moto.

Mwanaume anapomsotea mwanamke kwa muda mrefu, siku akimpata basi ni lazima mwanaume huyo kujikuta anashindwa kuucheza mchezo kiufundi na kujikuta kapanda mnazi na kuzdondosha zake kabala mwenzi wake hajafika popote.

Hata hivyo kua katika hali hii si ugonjwa bali ni hali ya kawaida tu ingawaje humfanya mmoja wenu kutofurahia na kujikuta akiwa na hamu ya kuendelea huku mwingine kachoka.pia kibaiolojia, tatizo hili linasababishwa na ukosefu wa uwiano wa “Homon” ikiwa homona zenu hazija zoeana, mwanaume anaweza kuona kuwa mwanamke hana ladha ile anayoitaka.

Sababu hiyo inaweza kumsababisha mwanaume kuvuta hisia kwa kumkimbuka mwanamke ambaye humfikisha na kumpa ladha anayoitaka ili aweze kukamilisha tendon a mwanake aliyenaye ka wakati huo hivyo anaweza akajikuta akilitaja jina la mwanamke mwingine wakati yuko na mwanamke mwingine.

Kisaikolojia hali ya kufika kileleni mapema bila mpangilio inasababisha na kushindwa kujiamini kwa mwanaume. Hapa ni kwa yule mwanaume aliyemsotea mwanamke kiasi cha kufikia hatua ya kukaribia kukata tama na baadae kujikuta kafanikiwa.

Mwanaume huyo huwa na kimuhemuhe cha kumpanda mwanamke huyo hivyo kujikuta kuwa amuonapo tu mrembo wake yeye anakuwa hahitaji tena maandalizi na ukimchekeweshea anaharibu mambo kabla ya kuanza kulili tunda lenyewe.

Kutokana na kutojiamini kwake, mwanuame huyo atakuwa akiwaza kama ni kweli ama ni ndoto kuwa na kimwana kama huyo aliye masotea kwa muda mrefuna sasa amefanikiwa kumuweka katika mikono yake, lazima mwanaume huyu atachetuka avuliwapo nguo na mwanadada huyu.

Kwa kawaida wanaume wengi hupenda wafanye mapenzi kwa dakika nyingi zaidi ili mwawa firahishe wapenzi wao lakini bila ya kutarajia wanajikuta wakiwa wamezidiwa nguvu na vimwana wao na hiyo ni kutokana na kuwa haijalishi kuwa ni muda gani maalumu wa mwanaume anatakiwa awe anafanya mapenzi kabla ya kufika kileleni.

Hebu tujiulize kwamba kuna ambaye anaweza kujizuia kufika kileleni mapema? Jibu ni kwamba unaweza ila cha msingi ni kuwa mtulivu na kuondfokana na wasiwasi, yaani unapaswa kujiamini kuwa unawza na umeshinda kuwa na huyo.

Usifanye mapenzi kwa kukomoa na wala usipanie sana kuwa lazima nikikutana na e niingie, jiamini kuwa ni wako na muda wote uko naye na unaweza kuchezanae upendavyo kwa kutumia muda wako.

Nimuhimu kujitambua kuwa utafika kileleni kwa wakati gani hivyo unaweza kujizuiakatika hatua hii muhimu kwa kujifunza na kuzoea.

Basi mpenzi msomaji wa safu hii napenda kukuaga kwa leo ila nakusihi tujumuike soto katika safu hii toleo lijalo.
Usultani Hadi Taifa Huru

Manispaa ya Zanzibar imegawanyika kihistoria katika maeneo mawili, nayo ni Mji Mkongwe na

Ng’ambo. Kuibuka na kukua kwa maeneo haya tangu karne ya 19, kumekuwa katika misingi ya

kiuchumi. Mji Mkongwe uliojengeka vema, ulikuwa kwa ajili ya matajiri na wasomi wakati viunga vya

Ng’ambo, vikawa kwa ajili ya walalahoi.

Mji Mkongwe ulianza kukua taratibu, awali kama makazi ya wavuvi kwenye Rasi ya Shangani katika

karne ya 12. Ulikuwa mji wa Kiswahili hasa, baadhi ya watu wakijishughulisha na sanaa za mikono, na

ikawa sehemu ya biashara zile ndefu zilizofanywa kwa njia ya bahari.

Kunako karne ya 17, Malkia Fatima alipotawala Unguja ya Kati, Mji wa Zanzibar uligeuka na kuwa

makao makuu ya falme yake. Alirithiwa na mwanawe Hasan, anayesemekana alifanya mengi katika

ujenzi wa Mji Mkongwe. Kuingia kwa wafanyabiashara wa Kireno pamoja na wale wa Kiarabu mwaka

1822, kulisababisha Waswahili kuhamia pande za mashariki mwa Mji Mkongwe.

Utawala wa Wareno ulipoanza kusambaratika katika Afrika Mashariki, Waarabu wa Oman, ambao awali

walikuja kama wafanyabiashara, walitwaa madaraka kisiwani Zanzibar. Waligeuza uchumi wa Zanzibar

kutegemea zaidi kilimo cha mashamba makubwa, ndipo uzalishaji wa karafuu ukashamiri na kukipatia

kisiwa umaarufu mkubwa. Japokuwa wamiliki ardhi hiyo walijenga nyumba mashambani, watu wengi

walipendelea zaidi makasri kandokando ya bahari, karibu na hekalu la Sultani.

Eneo ulipokuwa mji wa Zanzibar, lilikuwa jambo la umuhimu mkubwa, hasa wakati Sultani wa Oman,

Seyyid Said alipokuja Zanzibar na akaamua kuufanya kuwa makao makuu. Iliripotiwa kwamba idadi ya

watu kwenye mji huo ilikuwa kati ya 10,000 na 12,000.

Ujio wa Sultani Seyyid Said, ulileta zama mpya kwani mji huo uligeuka kuwa kituo kikuu cha biashara

katika Pwani ya Mashariki mwa Afrika. Misafara ya kibiashara ilistawi kwa kiasi kikubwa na yenye faida

pia, ikihusisha uuzaji watumwa kutoka pwani hii. Watumwa hao walitumiwa kuzalisha bidhaa

mbalimbali pamoja na dhahabu. Biashara ilistawi na misururu kutoka bara, ilileta pembe za ndovu,

dhahabu na watumwa ambao walifanya kazi kwenye mashamba hayo makubwa.

Ni mtawala huyo huyo ambaye aliweka misingi ya kuendeleza mji huu na pia, licha ya karafuu, mazao

mengine yaliyozalishwa kwa kiasi kikubwa ni minazi. Uzalishaji wa mazao haya ya biashara, ulisaidia

kukuza biashara, ikizingatiwa zaidi kwamba mji huu ulijaliwa kwa asili kuwa na bandari nzuri zaidi

kisiwani. Bandari iligeuka kuwa kituo kikuu cha usambazaji na pia kutoa mwelekeo kamili wa hali ya

biashara katika eneo hili.

Kwa vile mazingira yalikuwa mazuri kwa ajili ya shughuli za kibiashara, watu kutoka mashambani

walihamia mijini, wakisaka nafasi nzuri zaidi za ajira. Kwa misingi hiyo, ardhi ilihitajika kwa kiasi

kikubwa kwa sababu za kibiashara. Zama hizi, Waarabu, Wahindi na Wapersia, walidhibiti umiliki wa

ardhi kiasi cha kulazimisha wenyeji kununua ardhi kutoka kwa wamiliki wake kwa bei kubwa.

Kwa vile wakati huo hapakuwepo mipango mahususi ya kulinda na kudhibiti maendeleo ya makazi

mapya, ilifika hatua watu wakabuni makazi yasiyo na ramani kwenye eneo la Ng’ambo, jambo

lililosababisha makazi kuwa katika hali ya chini, kukosekana huduma za kijamii na miundombinu

muhimu.

Mwaka 1890, Zanzibar iliwekwa chini ya uangalizi wa Uingereza, Sultani akiwa bado na madaraka

makubwa ya kisiasa hata hivyo. Ni wakati huu ambapo, mipango mbalimbali ilianzishwa na chini ya

mpango huu, Waarabu waliendeleza maeneo ya Kidongo Chekundu, Sebleni, Kwahani na kadhalika.

Kabla ya uhuru, vyama kadhaa vya siasa tayari vilikuwa vikifanya kazi. Vyama vikuu vilikuwa Zanzibar

National Party (ZNP), kilitawaliwa zaidi na wasomi ambao ni wachumi. Chama kingine kilikuwa Afro

Shiraz (ASP), chama kilichokuwa na Waafrika wengi zaidi na kikiwa na mshikamano mkubwa wa

makundi ya wanyonge.

Katika uchaguzi wa mwisho kabla ya uhuru Julai mwaka 1963, ZNP kilichoshirikiana na chama kingine

kidogo cha Pemba, kilifanikiwa kupata wingi wa kura katika baraza jipya la kutunga sheria na Desemba

1963, Zanzibar ilikuwa huru kutoka kwa Waingereza. Mwezi mmoja baadaye, Januari 12 mwaka 1964,

serikali mpya ya Sultani iliangushwa baada ya kufanyika mapinduzi visiwani.

Sultani mwenyewe aliikimbia Zanzibar na ASP ikaingia madarakani na kuitawala nchi hadi mwaka 1977,

kilipoungana na wenzao wa Tanzania Bara, TANU na kuunda Chama Cha Mapinduzi (CCM) ambacho

hadi leo kipo madarakani. Licha ya kuwa sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Zanzibar

imekuwa na mamlaka makubwa ya kiserikali kujitawala, isipokuwa kwa masuala ya muungano. Masuala

hayo ya muungano ni kama vile ulinzi, sera za kigeni na mambo ya ndani. Zaidi ya hapo, Zanzibar inalo

Bunge lake, likijulikana zaidi kama Baraza la Wawakilishi lakini pia, inawakilishwa katika Bunge la Jamhuri

ya Muungano wa Tanzania, ikiwa na wabunge 50 huko.

Mwaka 1995, muswada ulipitishwa na kuwa sheria iliyoanzisha mfumo wa vyama vingi vya siasa na

katika uchaguzi wa kwanza, CCM ilishinda kama ilivyokuwa tena mwaka 2000 na uchaguzi wa tatu chini

ya mfumo huo utafanyika mwaka 2005.

Manispaa ya Zanzibar iko ndani ya eneo la Mjini Magharibi ambalo limegawanywa katika wilaya kuu

mbili; Wilaya ya Mjini na Wilaya ya Magharibi, kila moja ikiwa na mkuu wa wilaya aliyeteuliwa na rais.

Mipaka ya kiutawala kwa manispaa hii ni kama ile ya Wilaya ya Mjini. Hata hivyo, kwa mujibu wa

michoro iliyotokana na mipango ya mwaka 1982, Mji unachukua eneo kubwa zaidi ya mipaka ya

Manispaa na sehemu yake iko Wilaya ya Magharibi.

Halmashauri ya Manispaa pia, huendesha shughuli zake kwenye maeneo hayo ya Wilaya ya Magharibi,

ambayo kimsingi, yako nje ya mipaka ya awali (lakini ndani ya mipaka iliyowekwa kwa mipango ya Mji).

Mipaka hiyo mipya bado haijaidhinishwa na Wizara ya Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa kuwa ndiyo

mipaka rasmi ya manispaa.

Hali hii ya utata wa mipaka ya zamani na mipya, inasababisha mgongano kati ya taasisi na vikundi

nyingi. Kwa mfano, madiwani wa Wilaya ya Magharibi, hawapo kwenye Halmashauri ya Manispaa ya

Zanzibar (ZMC), japokuwa ZMC yenyewe inaendesha shughuli zake. Kwa vile mji umekua na kupanuka

zaidi ya manispaa, inaelekea haitachukua muda, mipaka ya manispaa yenyewe itabadilishwa. Kwa msingi

huo, ripoti hii kwa hiyo, inafuata mipaka mipya iliyopendekezwa na Tume ya Ardhi na Mazingira

(COLE) katika mpango ule wa mwaka 1982

Japokuwa idadi ya kata kwenye Wilaya ya Magharibi ni 10, tatu tu ndizo ziko ndani ya mipaka hii

mipya. Wilaya ya Mjini ina majimbo 13 wakati Wilaya ya Magharibi inazo tatu katika mipaka hiyo mipya.

Kila jimbo huwakilishwa na mbunge na mjumbe wa Baraza la Wawakilishi kwenye vyombo hivyo vya

kutunga sheria Zanzibar na katika Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kuna jumla ya kata 26 wilayani

Mjini Magharibi na tatu kwenye Wilaya ya Magharibi.

Kata hizo huwakilishwa kwenye Halmashauri ya Manispaa na madiwani wanaochaguliwa. Kwa sasa,

madiwani kutoka Wilaya ya Mjini ndio wanawawakilisha wananchi kwenye Baraza la Manispaa ya

Zanzibar.

Meya huchaguliwa kutoka miongoni mwa madiwani. Kata zimegawanywa tena katika shehia na kila

shehia ina kiongozi anayeitwa sheha. Wilaya ya Mjini ina shehia 39 wakati Wilaya ya Magharibi ina

shehia 23, sita zikiwa ndani ya mipango mipya ya mipaka. Japokuwa bado haijachapishwa kwenye

gazeti la serikali, kuna shehia mpya ya Karakana iliyoko Chumbuni, na hii inafanya jumla ya shehia kuwa

40

Zanzibar, ikijulikana zaidi kama visiwa vya marashi ya karafuu kutokana na sifa ya uzalishaji zao hilo,

inajumuisha visiwa viwili vikubwa ambavyo ni Unguja na Pemba. Manispaa ya Zanzibar iko katikati ya

Pwani ya Magharibi ya Kisiwa cha Unguja. Eneo hili lina ubapa kiasi, huku kukiwa na mwinuko kwa

upande wa magharibi, na kutoka Pwani, kuna mwinuko kidogo, kuelekea mashariki.

Kwa wastani, Pwani yenyewe iko meta 6.6 juu ya usawa wa bahari na eneo lililo lililoko chini zaidi ni

Tomondo, ambako kuna bonde lenye kina cha kati ya meta 10 hadi 15 chini ya usawa wa bahari

Eneo lililo juu zaidi ni tuta la Masingini, meta 100 kwa upande wa mashariki wakati kwa upande wa

magharibi, kuna visiwa vinne ambavyo ni Chapwani, Changuu, Kibandiko na visiwa vya Bawe (tazama

ramani 1.1):

Zanzibar iko kwenye ukanda wa kitropiki na mvua hutegemea kwa kiasi kikubwa majira na mabadiliko

ya pepo za Bahari ya Hindi. Masika ya Zanzibar huzalisha asilimia 40 ya mvua ya mwaka mzima na

huanza Machi hadi Mei. Kipindi cha ukavu, lakini chenye ubaridi kiasi kiitwacho Kusi, huanzia Juni na

kumalizika Septemba wakati Vuli yenye asilimia 20 ya mvua za mwaka mzima, huanzia Oktoba na

kumalizika Desemba. Kipindi cha pepo zitokazo kaskazini kwenda mashariki (Kaskazi), huanza Januari

na kumalizika Machi. mji huu hupata milimita 1,500 hadi 2,000 za mvua kwa mwaka.

Manispaa ya Zanzibar ndio makao makuu ya visiwa hivi na ndio kitovu chake kiuchumi, kisiasa na hata

kitamaduni. Hapa ndio makao makuu ya Serikali ya Mapinduzi Zanzibar. Huchangia kwa kiasi kikubwa

katika suala zima la biashara na utalii, sekta zinazochangia zaidi mapato ya fedha za kigeni.

Waweza kufika kwenye kisiwa hiki kupitia bandari au uwanja wa ndege wa kimataifa. Ni katika

manispaa hii ya Zanzibar pia, kuna sehemu muhimu kama vile ofisi za Serikali, sehemu za ibada,

biashara na zile za starehe na mapumziko.

Mpangilio wa makazi mjini hapa upo katika aina tano, na umetokana na mipango na taratibu tofauti

zilizoandaliwa (tazama ramani 1.2):

Mji Mkongwe uko upande wa magharibi wa barabara kuu. Ukiwa ndio bandari kongwe, inayotambulika

siku nyingi kihistoria, ina maeneo na majengo yaliyosanifiwa kwa aina yake na ni urithi wa kitamaduni

kwa Wazanzibari na pia ni kivutio kikubwa kabisa cha watalii.

N’gambo ni maeneo mengine makongwe, lakini ambayo hayajachorewa ramani. Yapo upande wa

mashariki wa barabara hiyo na yaliendelezwa kati ya mwaka 1840-1923. Maeneo yenyewe ni

Mwembetanga, Vikokotoni and Kiswandui.

Yapo maeneo mengine ya Ng’ambo yaliyofanyiwa michoro kiasi, kulingana na mipango na taratibu za

mwaka 1958. Maeneo haya ni pamoja na Kidongo Chekundu, Kwahani na Jang’ombe.

Maeneo mapya ambayo bado hayajapimwa, yaliendelezwa mara baada ya kuanzishwa kwa sera za

biashara huria. Haya ni pamoja na Chumbuni, Munduli, Darajabovu, Tomondo, Uholanzi na Kitosani.

Yapo maeneo mapya yaliyopimwa tayari. Maeneo haya yaliendelezwa baada ya michoro iliyoandaliwa

mwaka 1982 na maeneo yenyewe ni Mwanakwerekwe, Mombasa, Mpendae na Chukwani.

Utalii; Kitovu cha Maendeleo
Visiwa hivi vya marashi ya Karafuu, ni maarufu kwa fukwe zake maridadi, matumbawe
na mji wenyewe wa kihistoria; Mji Mkongwe. Kwa maana hiyo, utalii ni sekta muhimu
katika uchumi wa Zanzibar na huchangia asilimia 26 kwa pato la taifa na uchangiaji huo
unatarajiwa kukua kwa kati ya asilimia 5 na 10 kwa mwaka.
Manispaa ya Zanzibar ni injini muhimu zaidi katika sekta ya utalii. Mji huu ndio lango
kubwa la watalii, achilia mbali wenyewe kuwa kivutio. Kabla ya watalii kwenda pwani ya
mashariki, kwa kawaida hukaa kwa muda katika Mji Mkongwe kufurahia mandhari yake
(tazama ramani 2.1)
Moja Ya Sehemu Za Ufukwe Kisiwani Zanzibar
Mitaa myembamba ya mji huu, hali ya hewa iliyotulia, majengo ya kale, milangu
inayopendeza iliyochongwa kwa mtindo wa aina yake ya kuviringwa, maegesho na
fukwe ndivyo vitu vinavyowavutia zaidi watalii hapa. Mji huu Mkongwe unazo hoteli
nyingi, migahawa na maduka kwa watalii ambayo pia hutoa ajira kwa watu kutoka
Unguja, Pemba na hata Tanzania Bara.
Idadi ya hoteli zenye hadhi za kulaza wageni imeongezeka kwa kiasi kikubwa katika
kipindi cha miaka mitano iliyopita. Hata hivyo, hakuna uhakika wa hasa ni hoteli ngapi
zinazolaza watalii mjini hapa. Makadirio mengi yanaonyesha kwamba kuna vyumba
karibu 20,000 vya kulala kote kisiwani, na takriban asilimia 50 ya hizo, iko mjini.
Kamisheni ya Utalii ilirekodi ongezeko la asilimia 25 ya vyumba vinavyokodishwa kwa
watalii tangu mwaka 1987 hadi 1997. Jumla ya watalii walirekodiwa kuingia uwanja wa
ndege na kwenye bandari mbalimbali katika kipindi hicho, ni 587,640.
Sera ya Utalii Zanzibar imekuwa ikiegemea katika falsafa ya ubora wa hali ya juu na ujazo
mdogo wa watalii, mambo yanayoleta mapato makubwa kiuchumi kutoka kwenye sekta
hiyo, kwa ajili ya watu ambao ni wengi kisiwani, huku kukiwa na rasilimali chache.
Mwaka 1997, zaidi ya watalii 86,000 walitembelea Zanzibar wakati mwaka 1998, zaidi ya
watalii 100,000 walitarajiwa (tazama chati juu ya idadi ya watalii).
Japokuwa majengo ya kale hayapo Mji Mkongwe pekee, umaarufu wake unatokana
zaidi na kuwa mji wa kihistoria ambao pia ni makazi, ukiwa na majengo yenye
kupendeza, milango ya aina yake iliyoviringwa juu na kurembwa vilivyo, mitaa
myembamba ambayo watalii huishangaa na kufurahia sambamba na maisha ya jumla ya
Zanzibar.
Kivutio kingine kwa watalii ni rasilimali za bahari zilizopo. Ni kweli kwamba fukwe
zilizoko ndani ya Manispaa ya Zanzibar ni chache, visiwa vilivyo mbele ya mji, vina
matumbawe ya kupendeza ambayo ni maridhawa kwa ajili ya kuzamia na hata kupiga
mbizi. Uvuvi Kisiwani Zanzibar na Tabia Zake
Mazingira ya uvuvi Zanzibar ni ya kupendeza na inakadiriwa kwamba mwaka 1997, kiasi
cha watu 12,000 walirekodiwa kama wavuvi na vyombo vya uvuvi vilivyokuwepo wakati
huo ni 2,700.
Idadi kubwa ya watu (kwa mfano mwaka 1990, watu 6,000 kwa Pemba na Unguja),
hufanya kazi hutoa huduma katika sekta hii na huduma zihusianazo. Asilimia 22 ya
bajeti za kaya hutumika kununua samaki ambao ni chanzo kikubwa cha protini
Zanzibar, hasa kwa wale wenye kipato kidogo.
Manispaa ya Zanzibar ina vituo tisa vya kuvulia samaki ambavyo ni Malindi,
Malindi/jetty, Kizingo, Forodhani, Maruhubi, Kilimani, Mtoni, Mazizini na Bububu
(tazama ramani 2.3). Wastani wa samaki wanaovuliwa baharini katika maeneo ya Unguja
na kuletwa Manispaa ya Zanzibar ni takriban tani 2,273 kwa mwaka. Idadi ya samaki
wanaovuliwa kote Zanzibar ni kati ya tani 10,000 hadi 20,000 kwa mwaka na hii ni kwa
mujibu wa utafiti uliofanywa na Kamisheni ya Ardhi na Mazingira.
Wavuvi wenyeji hutumia karibu asilimia 96 ya samaki wanaowavua kwa soko la hapa
hapa, na wanaouzwa nje ni asilimia 4 tu. Kwa sasa, Manispaa ya Zanzibar ina kampuni
moja tu ya uvuvi iliyosajiliwa, yenyewe ikijulikana kama ZAFFICO. Ina waajiriwa wa
kudumu 60.
Wavuvi wengi wana vifaa duni na ndio sababu hasa ya uchache wa samaki wanaovuliwa.
Japokuwa takwimu zilizopo na za kuaminika hazitoshi, kuna vyanzo vinavyoonyesha
kwamba jumla ya idadi ya samaki waliopo kwenye maeneo haya, inapungua.

Uvuvi katika Manispaa ya Zanzibar unahusisha wale wavuvi wa asili na wengine ambao
wamekuja kufanya hivyo baadaye kwa sababu za kibiashara. Hawa wa asili,
wanaoonekana kama wasanii, hutumia vyombo vya uvuvi vya kijadi na mbinu za
kizamani, tofauti na wale wa kisasa ambao hutumia boti au vifaa vyenye injini.
Hawa wa asili huweza pia kutumia mishipi au fito na huweza kupata samaki wa
miambani na wa maji wazi kama kingfish na tuna. Wale wavuaji wa kibiashara zaidi
hupata samaki wa jamii ya bangala na wengine wadogo wadogo.
Samaki walioletwa Manispaa ya Zanzibar na kiasi chake kwa tani, thamani ikiwa katika
milioni za shilingiUchimbaji Zanzibar ni wa aina ndogo, ukilenga zaidi katika mchanga, mawe,
changarawe, chokaa na mchanga wa fukweni. Maeneo haya ya machimbo ni ya saizi
ndogo na ya kati na yamesambaa maeneo mbalimbali kisiwani.
Maeneo rasmi ya machimbo ni machache nje ya mipaka mipya ya mji, mmoja ukiwa ni
wa mchanga, katika eneo lenye ukubwa wa hekta mbili kwenye Wilaya ya Kaskazini B
na mengine mawili ya uchimbaji mawe na eneo moja la uchimbaji chokaa Wilaya ya
Magharibi. Mjini hakuna eneo rasmi la machimbo lakini hayo yaliyopo nje, hutumika
kwa ajili ya mji huu kwani inakadiriwa kwamba asilimia 90 ya yanayochimbwa huletwa
mjini.
Bidhaa hizo hutumika zaidi kwa ajili ya shughuli za ujenzi. Kuna maeneo mengine mengi
yasiyo rasmi, hasa kwa ajili ya kuchimba mchanga na ambayo hutumiwa ndani ya
manispaa, hasa katika maeneo jirani. Mchanga unachimbwa pia kinyume cha sheria
kwenye maeneo kama Mpiga Duri, Daraja Bovu, Amani, Welezo na Mpendae na
maeneo mengine kwenye kingo za mito. Ni vigumu kudhibiti hali hii kwani wachimbaji
hufanya kazi hiyo usiku. Jasi na udongo huchimbwa Mtoni, Chumbuni na Magogoni.
Ni kawaida kuona ngamia au ng’ombe dume wakibeba nyenzo hiyo vya ujenzi. Maeneo
yaliyoathirika zaidi ni Amaani, Magogoni na Maruhubi. Vitendo hivyo visivyo rasmi na
visivyoratibiwa katika Manispaa ya Zanzibar, vilisababisha mjadala mkali kwenye Baraza
la Wawakilishi kutokana na mmomonyoko wa ardhi. Japokuwa ilikubaliwa wizara husika
ichukue hatua, hali imebaki kuwa hivyo hivyo
Kilimo kimekuwa daima na umuhimu mkubwa kwa uchumi wa Zanzibar. Siku
zilizopita, uchumi ulitegemea kwa kiasi kikubwa mauzo ya karafuu na nazi nje ya nchi.
Hata hivyo, kupungua kwa bei kwenye masoko, kunaathiri kwa kiasi kikubwa mazao
hayo.
Katika Manispaa ya Zanzibar, kilimo kina mguso kidogo katika maendeleo ya mji.
Kilimo cha mjini ni kidogo, kama bustani tu na wajibu wa mji huu katika kilimo, ni kwa
vile tu mji huu ni soko kubwa kwa bidhaa za kilimo. Katika Mji Mkongwe hapafanyiki
kilimo, bali kinafanyika maeneo ya Ng’ambo lakini nako, kilimo kinashuka.
Maeneo ambayo kilimo kinafanyika zaidi ni Kilimani, Maruhubi, Saateni, Migombani -
Kaburi Kikombe, Kwaalinatu - Ziwani, Chumbuni, Mtoni, Kwahani na Sebleni, maeneo
yenye kiasi cha hekta 95. Mengi ya maeneo haya huzalisha chakula na mengine
yamegeuka kuwa mabwawa, hasa nyakati za mvua. Mpunga ndio zao kubwa linalolimwa
huko, likifuatiwa na ndizi na mboga kama vile spinachi, kabichi na nyinginezo. Katika
maeneo makavu kisiwani, viazi vitamu na mihogo hulimwa pia.
Maeneo haya yanatambuliwa rasmi na Wizara ya Kilimo, na wakazi hujitahidi kupanda,
japo miti michache ya matunda kwenye maeneo ya nyumba zao. Wengi wanaojihusisha
na kilimo cha mjini ni wanawake.
Mifugo kisiwani ipo pia, nayo ni kama ng’ombe, mbuzi, kuku, ngamia, bata na paka
ambao hupatikana maeneo ya Ng’ambo. Kuku na bata ndio wapo kwa wingi,
wakifuatiwa na ng’ombe na mbuzi. Maeneo ya Ng’ambo yenye mifugo mingi zaidi ni
Kiembe Samaki, Mwanakwerekwe, Mtoni, Bububu. Chukwani na Chumbuni.
Kwa sasa, mifugo katika kisiwa chote, huchangia asilimia 12 ya pato la taifa. Kuna
mipango ya kuboresha zaidi sekta hii ili kupunguza utapiamlo na pia kufikia mahitaji
halisi kwa wakazi wa mjini na sekta ya utalii. Kwa mujibu wa sensa ya mifugo ya mwaka
1993, kuna mifugo 73,000 katika visiwa vya Pemba na Unguja na kati ya hiyo, 13,000
ipo Wilaya za Mjini na Magharibi.
Katika maeneo ya kingo za mji, kwenye udongo wenye rutuba kwa ajili ya kilimo, ardhi
inagombewa kwa sababu mji nao unapanuka. Mashariki mwa mji, hasa maeneo
yaliyokuwa yakitumiwa kwa kilimo awali, sasa yanalazimika kuendelezwa kwa makazi.
Hali hii hupunguza maeneo ya uzalishaji chakula lakini pia husababisha mmonyoko wa
ardhi.
Kilimo kimekuwa daima na umuhimu mkubwa kwa uchumi wa Zanzibar. Siku zilizopita,
uchumi ulitegemea kwa kiasi kikubwa mauzo ya karafuu na nazi nje ya nchi. Hata hivyo,
kupungua kwa bei kwenye masoko, kunaathiri kwa kiasi kikubwa mazao hayo.
Katika Manispaa ya Zanzibar, kilimo kina mguso kidogo katika maendeleo ya mji.
Kilimo cha mjini ni kidogo, kama bustani tu na wajibu wa mji huu katika kilimo, ni kwa
vile tu mji huu ni soko kubwa kwa bidhaa za kilimo. Katika Mji Mkongwe hapafanyiki
kilimo, bali kinafanyika maeneo ya Ng’ambo lakini nako, kilimo kinashuka.
Maeneo ambayo kilimo kinafanyika zaidi ni Kilimani, Maruhubi, Saateni, Migombani -
Kaburi Kikombe, Kwaalinatu - Ziwani, Chumbuni, Mtoni, Kwahani na Sebleni, maeneo
yenye kiasi cha hekta 95. Mengi ya maeneo haya huzalisha chakula na mengine
yamegeuka kuwa mabwawa, hasa nyakati za mvua. Mpunga ndio zao kubwa linalolimwa
huko, likifuatiwa na ndizi na mboga kama vile spinachi, kabichi na nyinginezo. Katika
maeneo makavu kisiwani, viazi vitamu na mihogo hulimwa pia.
Maeneo haya yanatambuliwa rasmi na Wizara ya Kilimo, na wakazi hujitahidi kupanda,
japo miti michache ya matunda kwenye maeneo ya nyumba zao. Wengi wanaojihusisha
na kilimo cha mjini ni wanawake.
Mifugo kisiwani ipo pia, nayo ni kama ng’ombe, mbuzi, kuku, ngamia, bata na paka
ambao hupatikana maeneo ya Ng’ambo. Kuku na bata ndio wapo kwa wingi,
wakifuatiwa na ng’ombe na mbuzi. Maeneo ya Ng’ambo yenye mifugo mingi zaidi ni
Kiembe Samaki, Mwanakwerekwe, Mtoni, Bububu. Chukwani na Chumbuni.
Kwa sasa, mifugo katika kisiwa chote, huchangia asilimia 12 ya pato la taifa. Kuna
mipango ya kuboresha zaidi sekta hii ili kupunguza utapiamlo na pia kufikia mahitaji
halisi kwa wakazi wa mjini na sekta ya utalii. Kwa mujibu wa sensa ya mifugo ya mwaka
1993, kuna mifugo 73,000 katika visiwa vya Pemba na Unguja na kati ya hiyo, 13,000
ipo Wilaya za Mjini na Magharibi.
Katika maeneo ya kingo za mji, kwenye udongo wenye rutuba kwa ajili ya kilimo, ardhi
inagombewa kwa sababu mji nao unapanuka. Mashariki mwa mji, hasa maeneo
yaliyokuwa yakitumiwa kwa kilimo awali, sasa yanalazimika kuendelezwa kwa makazi.
Hali hii hupunguza maeneo ya uzalishaji chakula lakini pia husababisha mmonyoko wa
ardhi.
Utalii Ukiwezeshwa Tutaendelea
Na Aisha Mbaga
SERIKALI inaposhauriwa katika mabo yanayoendeleza nchi, nivyema ikatilia mkazo kwani wakati mwingine huwa ushauri unafaida kwa taifa,
kama tunakumbuka kipindi cha uongozi wa serikali ya Dk Salmin Amou, alitoa uamuzi wa kuruhusu sekta ya utalii Visiwani iendelezwe lakini mwanzoni uamuzi huo ukipingwa na wengi ikiwa ni pamoja na kulalamikiwa na baadhi ya wananchi ambao hawakuwa wakielewa vyema matokeo yake.
Kwa sasa wananchi wengi wanaona faida ya uamuzi huo na wengi wameuunga mkono kutokana na sekta hiyo kuleta matunda kwa wananchi wa Zanzibar na serikali kwa ujumla .
Rais Mstaafu Dk Salmin Amour na serikali yake walifikia uamuzi wa kuruhusu sekta ya utalii kuchipua mwaka 1992 kama njia ya kuongeza vyanzo vya mapato na kuinua hali za maisha ya wananchi wake.
Kutokana na umuhimu wa sekta hiyo, mwaka 1996, Dk Salmin aliamua kuanzisha kamisheni ya Utalii na kutunga sheria No. 9 ya mwaka 1996 ambayo inasimamia sekta hiyo.
Uamuzi huo, uliwashtua watu wengi na kupata upinzani wa chini kwa chini kwa vile faida zake zilikuwa hazionekani wakati huo.
Hatua hiyo, ilisababishwa na wasiwasi wa baadhi ya wananchi kuwa suala hilo linahusu mila na utamaduni, na kuhofia kuathirika kwa utamaduni wa Mzanzibari.
Hata hivyo malengo ya Dk. Salmin yalionekana tofauti na mawazo yao, kwa vile sekta hiyo hivi sasa imeleta faida kubwa kwa serikali na wananchi wake baada ya bei ya zao la karafuu kuporomoka katika soko la dunia.
Zao la karafuu lilitegemewa sana katika kuchangia pato la taifa tangu utawala wa kifalme wa Sultani na baada ya mapinduzi ya Zanzibar kwa vile mzunguko mkubwa wa fedha kwa wananchi wake ulitegemea zao hilo.
Mwenyeketi wa Kamisheni ya Utalii Zanzibar (ZTC) Issa Ahmed Othman anasema sekta ya utalii Zanzibar kwa sasa inachangia asilimia 20 ya pato la taifa kutokana na watalii wanaotembelea Zanzibar kutoka nchi mbalimbali duniani hasa Ulaya.
Anasema kuwa kuanzia mwezi wa Julai hadi Desemba mwaka jana, watalii wapatao 135,000 walitembelea Zanzibar, kiwango ambacho ni kikubwa kulinganishwa na watalii 125,443 waliotembea Zanzibar kipindi kama hicho mwaka 2005.
Alisema katika kipindi cha Januari pekee mwaka huu, watalii 14,117 walitembelea Zanzibar, kiwango ambacho hakijawahi kutokea katika kipindi cha mwezi mmoja kutembelewa na idadi kubwa ya watalii kama hiyo.
Mwenyekiti alisema kuwa, zipo sababu tatu za kuimarika sekta ya utalii Zanzibar, ikiwemo kwamba Zanzibar haina majanga ya kutisha, utulivu wa kisiasa, pamoja na kuwa na maeneo mengi yanayowavutia watalii.
Hata hivyo alisema, sekta hiyo inakabiliwa na matatizo makubwa mawili, kukosekana kwa watu wenye taaluma ya juu katika sekta ya utalii, kukosekana kwa soko la vyakula na matunda na hivyo kulazimika kutegemea kutoka nje ya Zanzibar.
``Sekta ya utalii ina tatizo la ukosefu wa watu wenye taaluma ya utalii na kulazimika nafasi nyingi kushikwa na watu kutoka nje ya Zanzibar,`` Akasema Mwenyekiti huyo.
Alisema kuwa, wakati Chuo cha Utalii Zanzibar- Maruhubi, kinatoa wanafunzi wenye kiwango cha cheti, uwekezaji wa utalii Zanzibar unakua na unahitaji watu wenye taaluma ya stashahada na shahada ya Chuo Kikuu.
Aidha alisema kwamba kumefika wakati Zanzibar iwe na shirika lake la ndege, kwa vile ina uwezo wa kulitumia soko hilo kwa watali wanao safari kati ya Zanzibar na mataifa ya Ulaya na Tanzania Bara.
``Watalii wanaosafiri kati ya Zanzibar na mikoa ya Tanzania Bara kuangalia vivutio vya utalii, bado hawana uhakika wa usafiri wa anga kwa vile ndege zinazotumika ni ndogo,`` Anasema Mwenyekiti.
Alisema kuwa, ni kweli Zanzibar ina mchango wake katika Shirika la Ndege la Tanzania (ATC) lakini tangu shirika hilo kubinafsishwa, na Serikali ya Muungano, limeimarisha zaidi safari zake kati ya Tanzania na Afrika Kusini wakati watalii wanatembelea Zanzibar wanatoka nchi za Magharibi na Ulaya.
Alisema kwamba, pamoja na mafanikio yaliyopatikana, sekta ya utalii Zanzibar inahitaji kuimarishwa katika sekta ya ulinzi ili kuwaondolea usumbufu watalii.
``Utaratibu wa kuwafanyia upekuzi watalii kwa kufungua mabegi yao na kuyapekua, umepitwa na wakati, lazima tuwe na vifaa vya kisasa ili tusiwapotezee muda wao wanapopita uwanja wa ndege,`` alisema Bw Othman.
Hata hivyo alisema ni kweli unapowakawiza wawekezaji, kuna faida na hasara lakini la msingi ni kuendelea kuheshimu mila na utamaduni.
``Unapokaribisha uwekezaji, ni sawa na kufungua dirisha, kila mdudu ataingia wakiwemo mbu na inzi. Cha msingi ni kuheshimu mila na utamaduni kama kweli tunataka kuwa na jamii bora `` Anasema Mwenyekiti huyo.
Akasema kwamba jambo la msingi lazima wanaume wakubali kubadili tabia, kwa vile wao ndio wanaoimarisha biashara ya ukahaba, na sio haki kuwachukulia hatua wanawake wanaojiuza kwa kutumia vibaya sekta ya utalii.
Aidha anasema kwamba, sekta ya utalii hadi hivi sasa inahitaji kuwa na mfumo mpya wa ukusanyaji mapato kutoka katika sekta hiyo ili takwimu sahihi ziwe zinapatikana.
Akasema kuwa hivi sasa vyombo ni vingi vinavyokusanya mapato, ikiwemo Bodi ya Mapato Zanzibar (ZRB), Baraza la Manispaa, Halmashauri za Wilaya, pamoja na jumuiya zisizokuwa za serikali zinazojishughulisha na sekta hiyo.
Anasema kwamba, sera ya utalii iliyopitishwa na wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, itafanikiwa kama taasisi zote za serikali zitaamuwa kuimarisha sekta za miundo mbinu, kilimo na uvuvi, ili Zanzibar iondoke katika kutegemea bidhaa za vyakula kutoka Tanzania bara katika soko hilo.
Kamishna wa Bodi ya Mapato Zanzibar, Bw Mohamed Ismail anasema kwamba wameamua kufanya ukaguzi usiku katika mahoteli ya kitalii baada ya kujitokeza vitendo vya udangayifu kwa wawekezaji.
Akasema kwamba maafisa wa bodi hiyo, wamekuwa wakifanya kazi saa 24, ikiwemo kukagua vyumba vya hoteli ambavyo havina wageni ili kuweka kumbukumbu sahihi za ulipaji kodi.
``Kuna baadhi ya wafanyabiashara, walikuwa wanapokea wageni 200 kwa siku, lakini wanalipia kiwango kidogo cha wageni, na utaratibu huu wa kufanya ukaguzi umetusaidia sana,`` Akasema kamishna Ismail.
Akasema kwamba, ukusanyaji wa mapato Zanzibar umeongezeka kwa asilimia 105.4 kutoka mwaka 1999 hadi mwaka wa fedha wa 2005/2006.
Akasema katika mwaka huu wa fedha bodi hiyo inatarajia kukusanya sh bilioni 60 kutoka sh bilioni 44.3 ambapo kila mwezi wanatarajiwa kukusanya sh bilioni tano badala ya sh bilioni 3.5.
Alisema kwamba, fedha hizo zinatoka katika vyanzo vitatu vya mapato ikiwemo sekta ya Utalii,mafuta na biashara.
Hata hivyo, baadhi ya wananchiZanzibar,wanasema sekta ya utalii Zanzibar imeyumbisha mila na utamaduni wa Mzanzibari kwa vile mavazi mengi wanaovaa vijana wakiwemo wasichana hayana tofauti na wanayovaa watalii wanayotoka nchi za ulaya.
``Zanzibar haikuwa rahisi kumuona msichana kavaa nguo fupi kitovu wazi,au nywele wazi, lakini hivi sasa ni vitu vya kawaida , na tunaamini hali hii imechangiwa na utandawazi katika sekta ya utalii,``Akasema Bw Abdulrahman Saleh mkazi wa Mkunazini.
Sheikh Suleiman Masoud wa Mtaa wa Kiponda anasema kuwa pamoja na sekta ya utalii kutoa mchango mkubwa, bado serikali inapasa kuwaeleimisha watalii wanapofika Zanzibar kuvaa nguo za heshima wanapotembelea mitaa mbalimbali hasa mji mkongwe.
``Tunaifundisha jamii yetu nini, kama wageni wanapita mitaani huku nguo za ndani zikionekana?
Tusijaribu kuacha utamaduni wetu, bado muda wa kuwaelimisha wageni upo,`` Akasema Zainab Kombo mkazi wa Vuga.
Pamoja na kuimarika kwa sekta ya Utalii Zanzibar, Serikali ya Mapinduzi Zanzibar(SMZ),bado inahitajika kuimarisha Chuo cha Utalii kilichopo Marhubi, ili vijana waweze kunufaika na sekta badala ya kuajiri vijana kutoka nchi jirani za Kenya, na Uganda.
Aidha sheria ya kazi No 3 ya mwaka 1997,na marekebisho yake lazima isimamiwe vizuri na kamisheni ya kazi Zanzibar ili iweze kuwanufaisha wafanyakazi wazalendo, ambao wana tofauti za mishahara kwa asilimia zaidi ya 80 na wafanyakazi wenzao wageni.
Pamoja na sheria hiyo, kuwapa uwezo maafisa wa kamisheni ya kazi kuhakikisha mikataba ya kazi wanaikagua kabla ya kufikiwa, kati ya wawekezaji na wafanyakazi wa kizalendo,lakini mikataba isiyozingatia sheria imeendelea kuwa kero katika sekta hiyo.
Wafanyakazi wengi wa kizalendo, wamekuwa wakifungishwa mikataba ya muda mfupi na kushindwa kunufaika na sheria ya mfuko wa Hifadhi wa Jamii Zanzibar,(ZSSF),kutopatiwa posho ya likizo, nyumba, matibabu, pamoja na malipo ya kazi za ziada.
WATOTO WAPEWE MALEZI BORA WAKUWE KIAKILI
Na Aisha Mbaga
WATOTO ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia
watoto wake, lakini vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi yao ni tatizo kubwa nchini
ambalolitaendelea kupigwa vita kila kukicha.
Mtu mmoja mmoja, familia au kaya na Serikali kwa ujumla wana jukumu la kuwalinda
watoto dhidi ya ukatili na unyanyasaji.
Hii inatokana na ukweli kwamba tatizo hilo limeota mizizi, kusambaa na kujichimbia
katika jamii ambapo kwa ujumla, usalama na ustawi wa watoto hapa nchini bado ni
tatizo.
Mwishoni mwa mwaka jana, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Kofi
Annan aliwasilisha katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa taarifa kuhusu utafiti juu ya
vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.
Tanzania ilishiriki katika utafiti huo kwa kuchangia taarifa mbalimbali katika dodoso
lililoandaliwa na Umoja wa Mataifa kwa udhamini uliofanywa na Ofisi ya Shirika la
Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) jijii Dar es Salaam ambayo
ilifadhili mradi wa utafiti uliofanywa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
katika wilaya 11 za Tanzania Bara.
Wilaya zilizofanyiwa utafiti huo ni Tabora, Morogoro Vijijini, Moshi Vijijini, Kilwa,
Mafia, Kibondo, Magu, Kinondoni, Lushoto, Mbinga na Mbeya.
Matokeo ya utafiti huo yalijadiliwa katika mkutano wa kitaifa wa wadau kuhusu namna
ya kuondokana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto uliofanyika
Oktoba 6 mwaka jana jijiini Dar es Salaam.
Wadau wa mkutano huo waliweka mikakati ya pamoja na kupiga vita vitendo hivyo
viovu vinavyofanywa dhidi ya watoto.
Pamoja na utafiti huo kufanyika katika wilaya 11, lakini ni ukweli usiofichika kuwa
yaliyobainika katika wilaya hizo chache, kwa kiasi kikubwa yanawakilisha taswira pana
ya tatizo hilo kwa nchi nzima.
Licha ya utafiti huo kuibua sababu nyingi za kuwepo kwa tatizo hili, hata hivyo ukweli
unaojitokeza ni kuwa hakuna sababu yo yote ile kati ya hizo inayoweza kuhalalisha
vitendo vya ukatili na unyanyasaji wanavyofanyiwa watoto.
Kwa upande Mwakilishi Mkazi wa UNICEF nchini, Bw. Rodney Philips anaona kuwa
ripoti ya utafiti huo imehimiza Serikali ya Tanzania kuwekeza raslimali na muda wa
kutosha katika kujenga uwezo, mtandao na ushirikiano wenye lengo la kupiga vita
vitendo vya udhalilishaji watoto vitakavyojitokeza kwa namna yo yote ile.
Akizungumza wakati akifungua mkutano huo, Rais Jakaya Kikwete alisema, `watoto
ndio msingi wa taifa la kesho, bila ya watoto kupewa malezi na matayarisho mazuri ni
wazi kuwa taifa halina matumaini mazuri siku za baadaye...watoto nchini ni wengi mno
kiasi kwamba tusipowaangalia na kuwaandaa au kuwaandalia vizuri ushiriki wao
wawapo vijana na watu wazima taifa litakuwa limepata hasara kubwa sana.`
Kwa mujibu wa sensa iliyotolewa na Idara ya Takwimu mwaka 2004 inaonyesha kuwa
hapa Tanzania watoto ni zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wote, yaani, zaidi ya nusu ya
Watanzania ni watoto na takwimu hizi zinaonyesha kuwa kwa wastani karibu kila kaya
nchini inao watoto wasiopungua sita.
Rais Kikwete alisema ni muhimu jamii itilie maanani ukweli huu na itambue watoto ni
sehemu muhimu ya jamii, siyo kwa idadi yao tu, bali pia kwa kuwa ni binadamu
wanaostahilil kupewa haki zote za msingi.
Ili kutekeleza vita dhidi ya tatizo hilo, viongozi wa Serikali, viongozi wa kidini, taasisi
mbalimbali, asasi zisizo za kiserikali, wananchi, watoto wanatakiwa kuweka mikakati
ya pamoja kwa lengo la kukomesha au kudhibiti vitendo viovu vinavyofanywa dhidi ya
watoto.
Bw. Philips anabainisha kuwa labda unyanyasaji mkubwa dhidi ya mtoto ni ule
unaofanywa na mtu mzima mwenye kuaminiwa na kupewa heshma na mtoto, lakini
anamgeuka na kumnyanyasa na kumdhalilisha kwa kumfanyia vitendo vya ngono.
Udhalilishaji wa watoto kimapenzi ni kitendo cha kuingilia undani wa mtoto,
udhalilishaji wa kimaumbile na kisaikolojia na uvunjaji mkubwa wa maadili na kanuni
za kijamii.
Bw. Philips ambaye alikuwa akizungumza katika mkutano wa kitaifa wa wadau
waliokuwa wakijadili Ripoti ya Unyanyasaji wa Mtoto Oktoba mwaka jana, alisema
jamii inatakiwa kuzuia vitendo vya kuwadhalilisha watoto ambao wamekuwa
wakianguka katika dimbwi la udhalilishaji wa kimapenzi mara kwa mara.
Alisema katika mambo yote hayo, jamii inatakiwa kuliangalia suala hilo kwa umakini
zaidi hasa kwa wasichana ambao wamekuwa wakiathirika zaidi katika udhalilishaji huo.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Mary Nagu anasema Tanzania itazingatia umuhimu wa
kuwa na sera madhubuti, sheria na kuwatambua watoto walio katika mazingira magumu.
Anataja umaskini, uharibifu wa mazingira na janga la Ukimwi kuwa ni maeneo
yanayohitaji nguvu ya pamoja kuyatokomeza ili watoto wawe na uhakika wa kukua na
kuishi maisha ya usalama.
Dk. Nagu anasema watoto ni zawadi kubwa kuliko zote kutoka kwa Mungu. Watoto ni
furaha ya kila aliye mzazi.
Watoto ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia watoto
wake, hivyo kuna kila ulazima wa kuwajenga na kuwalinda dhidi ya ukatili na
unyanyaswaji ili kuwahakikishia maisha yaliyo salama.
Kutokana na matokeo ya utafiti, usikilizaji hadharani, maoni na mapendekezo ya
wananchi na wadau mbalimbali kuhusu vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya
watoto, Tume ilianisha vitendo hivyo katika makundi manne ambayo ni; Unyanyasaji
kingono, Mashambulizi kimwili; Utelekezaji na Unyanyasaji wa kisaikolojia.
Katika maoni yake, Tume ilisema tatizo la unyanyasaji kingono linawaathiri zaidi
watoto wa kike kuliko wa kiume.
Utafiti huo umeonyesha kuwa sehemu kubwa ya wananchi na wadau wana uelewa wa
kutosha kuhusu aina hii ya unyanyasaji na inaonyesha ni suala linalowakera wananchi,
lakini vyombo vinavyohusika haviwajibiki ipasavyo.
Aidha baadhi ya wazazi/wananchi/walezi hawatekelezi wajibu wao ipasavyo katika
kulinda na kutetea watoto dhidi ya vitendo vya unyanyasaji kingono.
Kuhusu utelekezaji, Tume ilisema tatizo hilo limeonekana kuwa ni suala la familia
binafsi na huwaathiri watoto hao ambao ni taifa la kesho.
Imefahamika kuwa mzigo mkubwa wa kulea watoto katika familia maskini unabebwa
na kina mama. Unyanyasaji wa kisaikolojia una madhara makubwa kwa mtoto.
Hata Watoto ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia
watoto wake, lakini vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi yao ni tatizo kubwa nchini
ambalo litaendelea kupigwa vita kila kukicha.
Mtu mmoja mmoja, familia au kaya na Serikali kwa ujumla wana jukumu la kuwalinda
watoto dhidi ya ukatili na unyanyasaji.
Hii inatokana na ukweli kwamba tatizo hilo limeota mizizi, kusambaa na kujichimbia
katika jamii ambapo kwa ujumla, usalama na ustawi wa watoto hapa nchini bado ni
tatizo.
Mwishoni mwa mwaka jana, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Kofi
Annan aliwasilisha katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa taarifa kuhusu utafiti juu ya
vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.
Tanzania ilishiriki katika utafiti huo kwa kuchangia taarifa mbalimbali katika dodoso
lililoandaliwa na Umoja wa Mataifa kwa udhamini uliofanywa na Ofisi ya Shirika la
Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) jijii Dar es Salaam ambayo
ilifadhili mradi wa utafiti uliofanywa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
katika wilaya 11 za Tanzania Bara.
Wilaya zilizofanyiwa utafiti huo ni Tabora, Morogoro Vijijini, Moshi Vijijini, Kilwa,
Mafia, Kibondo, Magu, Kinondoni, Lushoto, Mbinga na Mbeya.
Matokeo ya utafiti huo yalijadiliwa katika mkutano wa kitaifa wa wadau kuhusu namna
ya kuondokana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto uliofanyika
Oktoba 6 mwaka jana jijiini Dar es Salaam.
Wadau wa mkutano huo waliweka mikakati ya pamoja na kupiga vita vitendo hivyo
viovu vinavyofanywa dhidi ya watoto.
Pamoja na utafiti huo kufanyika katika wilaya 11, lakini ni ukweli usiofichika kuwa
yaliyobainika katika wilaya hizo chache, kwa kiasi kikubwa yanawakilisha taswira pana
ya tatizo hilo kwa nchi nzima.
Licha ya utafiti huo kuibua sababu nyingi za kuwepo kwa tatizo hili, hata hivyo ukweli
unaojitokeza ni kuwa hakuna sababu yo yote ile kati ya hizo inayoweza kuhalalisha
vitendo vya ukatili na unyanyasaji wanavyofanyiwa watoto.
Kwa upande Mwakilishi Mkazi wa UNICEF nchini, Bw. Rodney Philips anaona kuwa
ripoti ya utafiti huo imehimiza Serikali ya Tanzania kuwekeza raslimali na muda wa
kutosha katika kujenga uwezo, mtandao na ushirikiano wenye lengo la kupiga vita
vitendo vya udhalilishaji watoto vitakavyojitokeza kwa namna yo yote ile.
Akizungumza wakati akifungua mkutano huo, Rais Jakaya Kikwete alisema, `watoto
ndio msingi wa taifa la kesho, bila ya watoto kupewa malezi na matayarisho mazuri ni
wazi kuwa taifa halina matumaini mazuri siku za baadaye...watoto nchini ni wengi mno
kiasi kwamba tusipowaangalia na kuwaandaa au kuwaandalia vizuri ushiriki wao
wawapo vijana na watu wazima taifa litakuwa limepata hasara kubwa sana.`
Kwa mujibu wa sensa iliyotolewa na Idara ya Takwimu mwaka 2004 inaonyesha kuwa
hapa Tanzania watoto ni zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wote, yaani, zaidi ya nusu ya
Watanzania ni watoto na takwimu hizi zinaonyesha kuwa kwa wastani karibu kila kaya
nchini inao watoto wasiopungua sita.
Rais Kikwete alisema ni muhimu jamii itilie maanani ukweli huu na itambue watoto ni
sehemu muhimu ya jamii, siyo kwa idadi yao tu, bali pia kwa kuwa ni binadamu
wanaostahilil kupewa haki zote za msingi.
Ili kutekeleza vita dhidi ya tatizo hilo, viongozi wa Serikali, viongozi wa kidini, taasisi
mbalimbali, asasi zisizo za kiserikali, wananchi, watoto wanatakiwa kuweka mikakati
ya pamoja kwa lengo la kukomesha au kudhibiti vitendo viovu vinavyofanywa dhidi ya
watoto.
Bw. Philips anabainisha kuwa labda unyanyasaji mkubwa dhidi ya mtoto ni ule
unaofanywa na mtu mzima mwenye kuaminiwa na kupewa heshma na mtoto, lakini
anamgeuka na kumnyanyasa na kumdhalilisha kwa kumfanyia vitendo vya ngono.
Udhalilishaji wa watoto kimapenzi ni kitendo cha kuingilia undani wa mtoto,
udhalilishaji wa kimaumbile na kisaikolojia na uvunjaji mkubwa wa maadili na kanuni
za kijamii.
Bw. Philips ambaye alikuwa akizungumza katika mkutano wa kitaifa wa wadau
waliokuwa wakijadili Ripoti ya Unyanyasaji wa Mtoto Oktoba mwaka jana, alisema
jamii inatakiwa kuzuia vitendo vya kuwadhalilisha watoto ambao wamekuwa
wakianguka katika dimbwi la udhalilishaji wa kimapenzi mara kwa mara.
Alisema katika mambo yote hayo, jamii inatakiwa kuliangalia suala hilo kwa umakini
zaidi hasa kwa wasichana ambao wamekuwa wakiathirika zaidi katika udhalilishaji huo.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Mary Nagu anasema Tanzania itazingatia umuhimu wa
kuwa na sera madhubuti, sheria na kuwatambua watoto walio katika mazingira magumu.
Anataja umaskini, uharibifu wa mazingira na janga la Ukimwi kuwa ni maeneo
yanayohitaji nguvu ya pamoja kuyatokomeza ili watoto wawe na uhakika wa kukua na
kuishi maisha ya usalama.
Dk. Nagu anasema watoto ni zawadi kubwa kuliko zote kutoka kwa Mungu. Watoto ni
furaha ya kila aliye mzazi.
Watoto ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia watoto
wake, hivyo kuna kila ulazima wa kuwajenga na kuwalinda dhidi ya ukatili na
unyanyaswaji ili kuwahakikishia maisha yaliyo salama.
Kutokana na matokeo ya utafiti, usikilizaji hadharani, maoni na mapendekezo ya
wananchi na wadau mbalimbali kuhusu vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya
watoto, Tume ilianisha vitendo hivyo katika makundi manne ambayo ni; Unyanyasaji
kingono, Mashambulizi kimwili; Utelekezaji na Unyanyasaji wa kisaikolojia.
Katika maoni yake, Tume ilisema tatizo la unyanyasaji kingono linawaathiri zaidi
watoto wa kike kuliko wa kiume.
Utafiti huo umeonyesha kuwa sehemu kubwa ya wananchi na wadau wana uelewa wa
kutosha kuhusu aina hii ya unyanyasaji na inaonyesha ni suala linalowakera wananchi,
lakini vyombo vinavyohusika haviwajibiki ipasavyo.
Aidha baadhi ya wazazi/wananchi/walezi hawatekelezi wajibu wao ipasavyo katika
kulinda na kutetea watoto dhidi ya vitendo vya unyanyasaji kingono.
Kuhusu utelekezaji, Tume ilisema tatizo hilo limeonekana kuwa ni suala la familia
binafsi na huwaathiri watoto hao ambao ni taifa la kesho.
Imefahamika kuwa mzigo mkubwa wa kulea watoto katika familia maskini unabebwa
na kina mama. Unyanyasaji wa kisaikolojia una madhara makubwa kwa mtoto.
Hata Watoto ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia
watoto wake, lakini vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi yao ni tatizo kubwa nchini
ambalo litaendelea kupigwa vita kila kukicha.
Mtu mmoja mmoja, familia au kaya na Serikali kwa ujumla wana jukumu la kuwalinda
watoto dhidi ya ukatili na unyanyasaji.
Hii inatokana na ukweli kwamba tatizo hilo limeota mizizi, kusambaa na kujichimbia
katika jamii ambapo kwa ujumla, usalama na ustawi wa watoto hapa nchini bado ni
tatizo.
Mwishoni mwa mwaka jana, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Kofi
Annan aliwasilisha katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa taarifa kuhusu utafiti juu ya
vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.
Tanzania ilishiriki katika utafiti huo kwa kuchangia taarifa mbalimbali katika dodoso
lililoandaliwa na Umoja wa Mataifa kwa udhamini uliofanywa na Ofisi ya Shirika la
Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) jijii Dar es Salaam ambayo
ilifadhili mradi wa utafiti uliofanywa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
katika wilaya 11 za Tanzania Bara.
Wilaya zilizofanyiwa utafiti huo ni Tabora, Morogoro Vijijini, Moshi Vijijini, Kilwa,
Mafia, Kibondo, Magu, Kinondoni, Lushoto, Mbinga na Mbeya.
Matokeo ya utafiti huo yalijadiliwa katika mkutano wa kitaifa wa wadau kuhusu namna
ya kuondokana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto uliofanyika
Oktoba 6 mwaka jana jijiini Dar es Salaam.
Wadau wa mkutano huo waliweka mikakati ya pamoja na kupiga vita vitendo hivyo
viovu vinavyofanywa dhidi ya watoto.
Pamoja na utafiti huo kufanyika katika wilaya 11, lakini ni ukweli usiofichika kuwa
yaliyobainika katika wilaya hizo chache, kwa kiasi kikubwa yanawakilisha taswira pana
ya tatizo hilo kwa nchi nzima.
Licha ya utafiti huo kuibua sababu nyingi za kuwepo kwa tatizo hili, hata hivyo ukweli
unaojitokeza ni kuwa hakuna sababu yo yote ile kati ya hizo inayoweza kuhalalisha
vitendo vya ukatili na unyanyasaji wanavyofanyiwa watoto.
Kwa upande Mwakilishi Mkazi wa UNICEF nchini, Bw. Rodney Philips anaona kuwa
ripoti ya utafiti huo imehimiza Serikali ya Tanzania kuwekeza raslimali na muda wa
kutosha katika kujenga uwezo, mtandao na ushirikiano wenye lengo la kupiga vita
vitendo vya udhalilishaji watoto vitakavyojitokeza kwa namna yo yote ile.
Akizungumza wakati akifungua mkutano huo, Rais Jakaya Kikwete alisema, `watoto
ndio msingi wa taifa la kesho, bila ya watoto kupewa malezi na matayarisho mazuri ni
wazi kuwa taifa halina matumaini mazuri siku za baadaye...watoto nchini ni wengi mno
kiasi kwamba tusipowaangalia na kuwaandaa au kuwaandalia vizuri ushiriki wao
wawapo vijana na watu wazima taifa litakuwa limepata hasara kubwa sana.`
Kwa mujibu wa sensa iliyotolewa na Idara ya Takwimu mwaka 2004 inaonyesha kuwa
hapa Tanzania watoto ni zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wote, yaani, zaidi ya nusu ya
Watanzania ni watoto na takwimu hizi zinaonyesha kuwa kwa wastani karibu kila kaya
nchini inao watoto wasiopungua sita.
Rais Kikwete alisema ni muhimu jamii itilie maanani ukweli huu na itambue watoto ni
sehemu muhimu ya jamii, siyo kwa idadi yao tu, bali pia kwa kuwa ni binadamu
wanaostahilil kupewa haki zote za msingi.
Ili kutekeleza vita dhidi ya tatizo hilo, viongozi wa Serikali, viongozi wa kidini, taasisi
mbalimbali, asasi zisizo za kiserikali, wananchi, watoto wanatakiwa kuweka mikakati
ya pamoja kwa lengo la kukomesha au kudhibiti vitendo viovu vinavyofanywa dhidi ya
watoto.
Bw. Philips anabainisha kuwa labda unyanyasaji mkubwa dhidi ya mtoto ni ule
unaofanywa na mtu mzima mwenye kuaminiwa na kupewa heshma na mtoto, lakini
anamgeuka na kumnyanyasa na kumdhalilisha kwa kumfanyia vitendo vya ngono.
Udhalilishaji wa watoto kimapenzi ni kitendo cha kuingilia undani wa mtoto,
udhalilishaji wa kimaumbile na kisaikolojia na uvunjaji mkubwa wa maadili na kanuni
za kijamii.
Bw. Philips ambaye alikuwa akizungumza katika mkutano wa kitaifa wa wadau
waliokuwa wakijadili Ripoti ya Unyanyasaji wa Mtoto Oktoba mwaka jana, alisema
jamii inatakiwa kuzuia vitendo vya kuwadhalilisha watoto ambao wamekuwa
wakianguka katika dimbwi la udhalilishaji wa kimapenzi mara kwa mara.
Alisema katika mambo yote hayo, jamii inatakiwa kuliangalia suala hilo kwa umakini
zaidi hasa kwa wasichana ambao wamekuwa wakiathirika zaidi katika udhalilishaji huo.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Mary Nagu anasema Tanzania itazingatia umuhimu wa
kuwa na sera madhubuti, sheria na kuwatambua watoto walio katika mazingira magumu.
Anataja umaskini, uharibifu wa mazingira na janga la Ukimwi kuwa ni maeneo
yanayohitaji nguvu ya pamoja kuyatokomeza ili watoto wawe na uhakika wa kukua na
kuishi maisha ya usalama.
Dk. Nagu anasema watoto ni zawadi kubwa kuliko zote kutoka kwa Mungu. Watoto ni
furaha ya kila aliye mzazi.
Watoto ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia watoto
wake, hivyo kuna kila ulazima wa kuwajenga na kuwalinda dhidi ya ukatili na
unyanyaswaji ili kuwahakikishia maisha yaliyo salama.
Kutokana na matokeo ya utafiti, usikilizaji hadharani, maoni na mapendekezo ya
wananchi na wadau mbalimbali kuhusu vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya
watoto, Tume ilianisha vitendo hivyo katika makundi manne ambayo ni; Unyanyasaji
kingono, Mashambulizi kimwili; Utelekezaji na Unyanyasaji wa kisaikolojia.
Katika maoni yake, Tume ilisema tatizo la unyanyasaji kingono linawaathiri zaidi
watoto wa kike kuliko wa kiume.
Utafiti huo umeonyesha kuwa sehemu kubwa ya wananchi na wadau wana uelewa wa
kutosha kuhusu aina hii ya unyanyasaji na inaonyesha ni suala linalowakera wananchi,
lakini vyombo vinavyohusika haviwajibiki ipasavyo.
Aidha baadhi ya wazazi/wananchi/walezi hawatekelezi wajibu wao ipasavyo katika
kulinda na kutetea watoto dhidi ya vitendo vya unyanyasaji kingono.
Kuhusu utelekezaji, Tume ilisema tatizo hilo limeonekana kuwa ni suala la familia
binafsi na huwaathiri watoto hao ambao ni taifa la kesho.
Imefahamika kuwa mzigo mkubwa wa kulea watoto katika familia maskini unabebwa
na kina mama. Unyanyasaji wa kisaikolojia una madhara makubwa kwa mtoto. Watoto ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia watoto
wake, lakini vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi yao ni tatizo kubwa nchini ambalo
litaendelea kupigwa vita kila kukicha.
Mtu mmoja mmoja, familia au kaya na Serikali kwa ujumla wana jukumu la kuwalinda
watoto dhidi ya ukatili na unyanyasaji.
Hii inatokana na ukweli kwamba tatizo hilo limeota mizizi, kusambaa na kujichimbia
katika jamii ambapo kwa ujumla, usalama na ustawi wa watoto hapa nchini bado ni
tatizo.
Mwishoni mwa mwaka jana, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Kofi
Annan aliwasilisha katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa taarifa kuhusu utafiti juu ya
vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.
Tanzania ilishiriki katika utafiti huo kwa kuchangia taarifa mbalimbali katika dodoso
lililoandaliwa na Umoja wa Mataifa kwa udhamini uliofanywa na Ofisi ya Shirika la
Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) jijii Dar es Salaam ambayo
ilifadhili mradi wa utafiti uliofanywa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
katika wilaya 11 za Tanzania Bara.
Wilaya zilizofanyiwa utafiti huo ni Tabora, Morogoro Vijijini, Moshi Vijijini, Kilwa,
Mafia, Kibondo, Magu, Kinondoni, Lushoto, Mbinga na Mbeya.
Matokeo ya utafiti huo yalijadiliwa katika mkutano wa kitaifa wa wadau kuhusu namna
ya kuondokana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto uliofanyika
Oktoba 6 mwaka jana jijiini Dar es Salaam.
Wadau wa mkutano huo waliweka mikakati ya pamoja na kupiga vita vitendo hivyo
viovu vinavyofanywa dhidi ya watoto.
Pamoja na utafiti huo kufanyika katika wilaya 11, lakini ni ukweli usiofichika kuwa
yaliyobainika katika wilaya hizo chache, kwa kiasi kikubwa yanawakilisha taswira pana
ya tatizo hilo kwa nchi nzima.
Licha ya utafiti huo kuibua sababu nyingi za kuwepo kwa tatizo hili, hata hivyo ukweli
unaojitokeza ni kuwa hakuna sababu yo yote ile kati ya hizo inayoweza kuhalalisha
vitendo vya ukatili na unyanyasaji wanavyofanyiwa watoto.
Kwa upande Mwakilishi Mkazi wa UNICEF nchini, Bw. Rodney Philips anaona kuwa
ripoti ya utafiti huo imehimiza Serikali ya Tanzania kuwekeza raslimali na muda wa
kutosha katika kujenga uwezo, mtandao na ushirikiano wenye lengo la kupiga vita
vitendo vya udhalilishaji watoto vitakavyojitokeza kwa namna yo yote ile.
Akizungumza wakati akifungua mkutano huo, Rais Jakaya Kikwete alisema, `watoto
ndio msingi wa taifa la kesho, bila ya watoto kupewa malezi na matayarisho mazuri ni
wazi kuwa taifa halina matumaini mazuri siku za baadaye...watoto nchini ni wengi mno
kiasi kwamba tusipowaangalia na kuwaandaa au kuwaandalia vizuri ushiriki wao
wawapo vijana na watu wazima taifa litakuwa limepata hasara kubwa sana.`
Kwa mujibu wa sensa iliyotolewa na Idara ya Takwimu mwaka 2004 inaonyesha kuwa
hapa Tanzania watoto ni zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wote, yaani, zaidi ya nusu ya
Watanzania ni watoto na takwimu hizi zinaonyesha kuwa kwa wastani karibu kila kaya
nchini inao watoto wasiopungua sita.
Rais Kikwete alisema ni muhimu jamii itilie maanani ukweli huu na itambue watoto ni
sehemu muhimu ya jamii, siyo kwa idadi yao tu, bali pia kwa kuwa ni binadamu
wanaostahilil kupewa haki zote za msingi.
Ili kutekeleza vita dhidi ya tatizo hilo, viongozi wa Serikali, viongozi wa kidini, taasisi
mbalimbali, asasi zisizo za kiserikali, wananchi, watoto wanatakiwa kuweka mikakati
ya pamoja kwa lengo la kukomesha au kudhibiti vitendo viovu vinavyofanywa dhidi ya
watoto.
Bw. Philips anabainisha kuwa labda unyanyasaji mkubwa dhidi ya mtoto ni ule
unaofanywa na mtu mzima mwenye kuaminiwa na kupewa heshma na mtoto, lakini
anamgeuka na kumnyanyasa na kumdhalilisha kwa kumfanyia vitendo vya ngono.
Udhalilishaji wa watoto kimapenzi ni kitendo cha kuingilia undani wa mtoto,
udhalilishaji wa kimaumbile na kisaikolojia na uvunjaji mkubwa wa maadili na kanuni
za kijamii.
Bw. Philips ambaye alikuwa akizungumza katika mkutano wa kitaifa wa wadau
waliokuwa wakijadili Ripoti ya Unyanyasaji wa Mtoto Oktoba mwaka jana, alisema
jamii inatakiwa kuzuia vitendo vya kuwadhalilisha watoto ambao wamekuwa
wakianguka katika dimbwi la udhalilishaji wa kimapenzi mara kwa mara.
Alisema katika mambo yote hayo, jamii inatakiwa kuliangalia suala hilo kwa umakini
zaidi hasa kwa wasichana ambao wamekuwa wakiathirika zaidi katika udhalilishaji huo.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Mary Nagu anasema Tanzania itazingatia umuhimu wa
kuwa na sera madhubuti, sheria na kuwatambua watoto walio katika mazingira magumu.
Anataja umaskini, uharibifu wa mazingira na janga la Ukimwi kuwa ni maeneo
yanayohitaji nguvu ya pamoja kuyatokomeza ili watoto wawe na uhakika wa kukua na
kuishi maisha ya usalama.
Dk. Nagu anasema watoto ni zawadi kubwa kuliko zote kutoka kwa Mungu. Watoto ni
furaha ya kila aliye mzazi.
Watoto ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia watoto
wake, hivyo kuna kila ulazima wa kuwajenga na kuwalinda dhidi ya ukatili na
unyanyaswaji ili kuwahakikishia maisha yaliyo salama.
Kutokana na matokeo ya utafiti, usikilizaji hadharani, maoni na mapendekezo ya
wananchi na wadau mbalimbali kuhusu vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya
watoto, Tume ilianisha vitendo hivyo katika makundi manne ambayo ni; Unyanyasaji
kingono, Mashambulizi kimwili; Utelekezaji na Unyanyasaji wa kisaikolojia.
Katika maoni yake, Tume ilisema tatizo la unyanyasaji kingono linawaathiri zaidi
watoto wa kike kuliko wa kiume.
Utafiti huo umeonyesha kuwa sehemu kubwa ya wananchi na wadau wana uelewa wa
kutosha kuhusu aina hii ya unyanyasaji na inaonyesha ni suala linalowakera wananchi,
lakini vyombo vinavyohusika haviwajibiki ipasavyo.
Aidha baadhi ya wazazi/wananchi/walezi hawatekelezi wajibu wao ipasavyo katika
kulinda na kutetea watoto dhidi ya vitendo vya unyanyasaji kingono.
Kuhusu utelekezaji, Tume ilisema tatizo hilo limeonekana kuwa ni suala la familia
binafsi na huwaathiri watoto hao ambao ni taifa la kesho.
Imefahamika kuwa mzigo mkubwa wa kulea watoto katika familia maskini unabebwa
na kina mama. Unyanyasaji wa kisaikolojia una madhara makubwa kwa mtoto.
Watoto ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia watoto
wake, lakini vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi yao ni tatizo kubwa nchini ambalo
litaendelea kupigwa vita kila kukicha.
Mtu mmoja mmoja, familia au kaya na Serikali kwa ujumla wana jukumu la kuwalinda
watoto dhidi ya ukatili na unyanyasaji.
Hii inatokana na ukweli kwamba tatizo hilo limeota mizizi, kusambaa na kujichimbia
katika jamii ambapo kwa ujumla, usalama na ustawi wa watoto hapa nchini bado ni
tatizo.
Mwishoni mwa mwaka jana, aliyekuwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Bw. Kofi
Annan aliwasilisha katika Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa taarifa kuhusu utafiti juu ya
vitendo vya ukatili dhidi ya watoto.
Tanzania ilishiriki katika utafiti huo kwa kuchangia taarifa mbalimbali katika dodoso
lililoandaliwa na Umoja wa Mataifa kwa udhamini uliofanywa na Ofisi ya Shirika la
Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (UNICEF) jijii Dar es Salaam ambayo
ilifadhili mradi wa utafiti uliofanywa na Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora
katika wilaya 11 za Tanzania Bara.
Wilaya zilizofanyiwa utafiti huo ni Tabora, Morogoro Vijijini, Moshi Vijijini, Kilwa,
Mafia, Kibondo, Magu, Kinondoni, Lushoto, Mbinga na Mbeya.
Matokeo ya utafiti huo yalijadiliwa katika mkutano wa kitaifa wa wadau kuhusu namna
ya kuondokana na vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya watoto uliofanyika
Oktoba 6 mwaka jana jijiini Dar es Salaam.
Wadau wa mkutano huo waliweka mikakati ya pamoja na kupiga vita vitendo hivyo
viovu vinavyofanywa dhidi ya watoto.
Pamoja na utafiti huo kufanyika katika wilaya 11, lakini ni ukweli usiofichika kuwa
yaliyobainika katika wilaya hizo chache, kwa kiasi kikubwa yanawakilisha taswira pana
ya tatizo hilo kwa nchi nzima.
Licha ya utafiti huo kuibua sababu nyingi za kuwepo kwa tatizo hili, hata hivyo ukweli
unaojitokeza ni kuwa hakuna sababu yo yote ile kati ya hizo inayoweza kuhalalisha
vitendo vya ukatili na unyanyasaji wanavyofanyiwa watoto.
Kwa upande Mwakilishi Mkazi wa UNICEF nchini, Bw. Rodney Philips anaona kuwa
ripoti ya utafiti huo imehimiza Serikali ya Tanzania kuwekeza raslimali na muda wa
kutosha katika kujenga uwezo, mtandao na ushirikiano wenye lengo la kupiga vita
vitendo vya udhalilishaji watoto vitakavyojitokeza kwa namna yo yote ile.
Akizungumza wakati akifungua mkutano huo, Rais Jakaya Kikwete alisema, `watoto
ndio msingi wa taifa la kesho, bila ya watoto kupewa malezi na matayarisho mazuri ni
wazi kuwa taifa halina matumaini mazuri siku za baadaye...watoto nchini ni wengi mno
kiasi kwamba tusipowaangalia na kuwaandaa au kuwaandalia vizuri ushiriki wao
wawapo vijana na watu wazima taifa litakuwa limepata hasara kubwa sana.`
Kwa mujibu wa sensa iliyotolewa na Idara ya Takwimu mwaka 2004 inaonyesha kuwa
hapa Tanzania watoto ni zaidi ya asilimia 50 ya wananchi wote, yaani, zaidi ya nusu ya
Watanzania ni watoto na takwimu hizi zinaonyesha kuwa kwa wastani karibu kila kaya
nchini inao watoto wasiopungua sita.
Rais Kikwete alisema ni muhimu jamii itilie maanani ukweli huu na itambue watoto ni
sehemu muhimu ya jamii, siyo kwa idadi yao tu, bali pia kwa kuwa ni binadamu
wanaostahilil kupewa haki zote za msingi.
Ili kutekeleza vita dhidi ya tatizo hilo, viongozi wa Serikali, viongozi wa kidini, taasisi
mbalimbali, asasi zisizo za kiserikali, wananchi, watoto wanatakiwa kuweka mikakati
ya pamoja kwa lengo la kukomesha au kudhibiti vitendo viovu vinavyofanywa dhidi ya
watoto.
Bw. Philips anabainisha kuwa labda unyanyasaji mkubwa dhidi ya mtoto ni ule
unaofanywa na mtu mzima mwenye kuaminiwa na kupewa heshma na mtoto, lakini
anamgeuka na kumnyanyasa na kumdhalilisha kwa kumfanyia vitendo vya ngono.
Udhalilishaji wa watoto kimapenzi ni kitendo cha kuingilia undani wa mtoto,
udhalilishaji wa kimaumbile na kisaikolojia na uvunjaji mkubwa wa maadili na kanuni
za kijamii.
Bw. Philips ambaye alikuwa akizungumza katika mkutano wa kitaifa wa wadau
waliokuwa wakijadili Ripoti ya Unyanyasaji wa Mtoto Oktoba mwaka jana, alisema
jamii inatakiwa kuzuia vitendo vya kuwadhalilisha watoto ambao wamekuwa
wakianguka katika dimbwi la udhalilishaji wa kimapenzi mara kwa mara.
Alisema katika mambo yote hayo, jamii inatakiwa kuliangalia suala hilo kwa umakini
zaidi hasa kwa wasichana ambao wamekuwa wakiathirika zaidi katika udhalilishaji huo.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Mary Nagu anasema Tanzania itazingatia umuhimu wa
kuwa na sera madhubuti, sheria na kuwatambua watoto walio katika mazingira magumu.
Anataja umaskini, uharibifu wa mazingira na janga la Ukimwi kuwa ni maeneo
yanayohitaji nguvu ya pamoja kuyatokomeza ili watoto wawe na uhakika wa kukua na
kuishi maisha ya usalama.
Dk. Nagu anasema watoto ni zawadi kubwa kuliko zote kutoka kwa Mungu. Watoto ni
furaha ya kila aliye mzazi.
Watoto ni mategemeo na matumaini ya wazazi na taifa lo lote linajengwa kupitia watoto
wake, hivyo kuna kila ulazima wa kuwajenga na kuwalinda dhidi ya ukatili na
unyanyaswaji ili kuwahakikishia maisha yaliyo salama.
Kutokana na matokeo ya utafiti, usikilizaji hadharani, maoni na mapendekezo ya
wananchi na wadau mbalimbali kuhusu vitendo vya ukatili na unyanyasaji dhidi ya
watoto, Tume ilianisha vitendo hivyo katika makundi manne ambayo ni; Unyanyasaji
kingono, Mashambulizi kimwili; Utelekezaji na Unyanyasaji wa kisaikolojia.
Katika maoni yake, Tume ilisema tatizo la unyanyasaji kingono linawaathiri zaidi
watoto wa kike kuliko wa kiume.
Utafiti huo umeonyesha kuwa sehemu kubwa ya wananchi na wadau wana uelewa wa
kutosha kuhusu aina hii ya unyanyasaji na inaonyesha ni suala linalowakera wananchi,
lakini vyombo vinavyohusika haviwajibiki ipasavyo.
Aidha baadhi ya wazazi/wananchi/walezi hawatekelezi wajibu wao ipasavyo katika
kulinda na kutetea watoto dhidi ya vitendo vya unyanyasaji kingono.
Kuhusu utelekezaji, Tume ilisema tatizo hilo limeonekana kuwa ni suala la familia
binafsi na huwaathiri watoto hao ambao ni taifa la kesho.
Imefahamika kuwa mzigo mkubwa wa kulea watoto katika familia maskini unabebwa
na kina mama. Unyanyasaji wa kisaikolojia una madhara makubwa kwa mtoto.
Hata akiwa mtu mzima, madhara hayo huendelea iwapo hayatapata ufumbuzi kama vile
matukio ya watoto kuchanganywa gerezani/mahabusu na watuu wazima hayamrekebishi
mtoto bali yanaongeza utukufu na usugu.
Serikali isikae kimya na kuachia hali hiyo ikiendelea, lazima ichukue hatua kali kwa
mujibu wa sheria kwa wale wote ambao wanaendeleza vitendo vya ukatili na
unyanyasaji kwa watoto.
Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, kama chombo cha kitaifa cha kutetea,
kueneza na kulinda haki za binadamu na misingi ya utawala bora nchini imekuwa
ikifuatilia kwa makini suala la haki za makundi maalumu, ikiwa ni pamoja na kundi la
watoto.
mwisho


SIGARA INAMADHARA KULIKO MOSHI WA GARI

Na aisha Mbaga
Uvutaji sigara umekuwa kama kitu cha kawaida kwa watu wengi. Watu huvuta sigara
ili kujisikia vizuri, kuchangamka, kupunguza mawazo na wengine huvuta kama
sehemu ya starehe.
Lakini, sigara au tumbaku hufanya nini miilini mwetu? Je unajua kuwa moshi wa
sigara una madhara kuliko hewa inayotoka kwenye injini za magari?
Dk. Phiilipo Kinabo wa hospitali ya Muzdalfa Yombo Vituka, anasema kuwa, wavutaji
wengi wa Sugara wamekuwa na sfya mbaya kutokana na kuathurika kwa mapafu
hivyo kusumbuliwa na ugonjwa wa TB na kusababisha vifo vingi zaidi.
Kinabo alisema kuwa, wanaoathirika zaidi ni vijana ambao wameshindwa kuacha japo
hawakuanza kuvuta kwa sababu ni dawa ama sigara inavurutubishi, lahasha , wengi
wameathirika kwa tabia za kuiga na kuhisi kuwa wanaovuta sigara ni waungwana
kuliko walevi.
pia alisema kuwa, hakuna kitu kibaya chenye kutoa moshi kinachodhuru kama moshi
wa sigara kutokana na madhara yake kuwa hasara kwa taifa. "Nashidwa kujua kwanini
Serikali inashindwa kupiga marufuku utengenezwaji wa sigara wakati inafahamu wazi
kuwa sigara inahatarisha maisha ya wanadamu wengi Diniana kote.
"Tumbaku ni jani lenye sumu aina ya nicotine ambalo hutafunwa au kuvutwa.
Tumbaku inachangamsha mwili kama ilivyo kwa sumu aina ya caffeine, ambayo
hupatikana kwenye kahawa au chai. Sumu hii, humfanya mtumiaji aizoee kwa haraka
sana. Inamchangamsha mtumiaji na kumfanya awe macho wakati mwingi. Haileweshi
lakini inapunguza hamu ya kula," alisema Dk. Kinabo
pia aliongezea kuwa Uvutaji sigara, unapunguza hewa ya oksijeni kutoka mwilini mwa
mvutaji na kusababisha mwili kutofanya kazi vizuri. Moshi wake unaharibu mishipa na
kusababisha shinikizo la damu na matatizo mengine ya moyo.
"Tumbaku ina lami, ambayo husababisha mapafu kutojisafisha vizuri na kuchangia
kupata maradhi kama vile saratani ya mapafu au koo. Huharibu ngozi na kuathiri
viumbe ambavyo havijazaliwa,"alisma Kinabo.
pia alieleza kuwa, pale mvutaji anapojikuta amekuwa mzoefu inamuwia vigumu
kuacha sigara kutokana na hali halisi, "wengi hujaribu kuacha lakini hushindwa na
kukosa raha, usingizi na kushindwa kufikiri vizuri" alisema Dk. Kinabo.
"Sumu iliyopo kwenye sigara ina madhara makubwa kwa afya. Serikali kwa kutambua
hilo, huwalazimisha watengenezaji wa sigara, kuweka onyo kali la tahadhari kwenye
paketi zao lakini hiyo haitoshi kwani bado watavuta hivyo ni vyema ikapigwa marufuku
kama ilivyo kwa bangi na mihadarati mingine," alieleza Kinabo.
"Kiungo rahisi kuathirika katika uvutaji wa sigara ni mapafu. Baada ya kuvuta moshi
wa kaboni na tindikali iliyomo kwenye tumbaku huishia kwenye mapafu ambavyo
husababisha ugumu katika kupumua na kusababisha kutunga usaha kwenye
mapafu"alisema.
"Hii huchangia kupata maambukizi mengine kama kichomi, kifua kikuu na saratani.
Nikotini vilevile ni mbaya kwa tumbo na husababisha kupoteza hamu ya kula na
maumivu katika tumbo. Watu wanaovuta mara kwa mara hutoa harufu mbaya
mdomoni na hupata matatizo ya ngozi", aliseleza Dk huyo wa mapafu.
Akilinganisha moshi wa sigara na mwingineo barabarani, twaweza kujiuliza. "Je, hewa
chafu na yenye moshi wa sigara ndani ya baa ikilinganishwa na barabarani, ambako
kuna hewa nyingi zinazotoka kwenye injini za magari, kipi kina madhara zaidi", alihoji?
Utafiti uliofanywa na wataalamu huko Marekani umedhihirisha kuwa hewa ya ndani ya
baa ina madhara zaidi. Na uchafuzi kwa hewa ya ndani ya baa au majumba ya
burudani, hautaweza kuondolewa kama watu hawatazuiwa kuvuta sigara ndani ya
majengo hayo.
Matokeo ya utafiti huo, yameonesha kuwa ikilinganishwa na ubora wa hewa iliyoko
katika barabara ambazo magari huenda kwa kasi au zile za mijini, wakati ambao kuna
msongamano wa magari, hewa iliyoko katika baa au majumba ya burudani ina
chembechembe nyingi zinazoweza kusababisha ugonjwa wa saratani kwa zaidi ya
mara hamsini.
Bw. Jeams Rapaz ni kiongozi aliyeongoza utafiti huo. Kwa mara ya kwanza aligundua
kuwa, moshi unaotoka kwenye sigara unasababisha maelfu ya watu kufariki dunia kila
mwaka.
Katika utafiti huo, Bw. Jeams Rapaz aliona kuwa, kiwango cha chembechembe
ndogo zenye uchafuzi wa mazingira katika maeneo wanakofanya kazi wafanyakazi
wa majumba ya starehe na migahawa ni cha juu sana kuliko kiwango cha uchafuzi
kinachoruhusiwa katika hewa ya nje ya majengo.
Kati ya mwezi Novemba mwaka 2002 na Januari mwaka 2003, Bw. Jean Rapaz
alifanya uchunguzi kuhusu hali ya hewa katika majumba ya starehe na migahawa sita
ya mkoani Delaware na kupima chembe za aina mbili zilizoko katika moshi wa sigara.
Matokeo yake yalionesha kuwa kuna microgram mia mbili na thelathini na moja za
chembechembe katika kila mita za ujazo, kiasi ambacho ni mara kumi na tano kuliko
kikomo cha chembe kinachoruhusiwa na mamlaka ya mazingira nchini Marekani.
Na ni mara arobaini na tisa kuliko chembe zilizoko katika barabara ya kasi ya
Wilmington, Marekani wakati wenye msongamano wa magari.
Chembe za uchafuzi za aina mbili, zenye madhara kwa afya za watu zilizoko katika
moshi wa sigara ndani ya majengo manane ya burudani wakati wa usiku zilikuwa na
microgram mia moja thelathini na nne, kiasi ambacho ni mara tano kuliko kikomo
kinachoruhusiwa katika hewa ya nje ya majengo.
Ingawa barabara ya kasi ya Wilmington, ambako kuna uchafuzi mwingi ndani ya hewa
zinazotoka kwenye injini za magari wakati wa msongamano wa magari, lakini chembe
za aina hizo ndani ya hewa ya huko ni microgram saba tu.
Kupiga marufuku kuvuta sigara ndani ya majengo, hususan katika majengo ya
burudani na migahawa ni njia nzuri. Utafiti uliofanywa umeonesha kuwa baada ya
kutolewa amri ya kupiga marufuku kuvuta sigara ndani ya majengo, chembechembe
za aina hizo zenye uchafuzi katika hewa ya majengo ya burudani yaliyotajwa hapo juu,
zimepungua kwa asilimia 90.
Utekelezaji wa sheria ya matumizi ya tumbaku na bidhaa zake nchini Marekani
adhabu dhidi ya matumizi inaanzia sh 56,250 mpaka sh milioni 1.2 au jela miezi sita
kwa wavutaji na wamiliki wa sehemu zinazovunja sheria hiyo.
Tunapaswa kujiuliza kama sheria ya udhibiti wa bidhaa za tumbaku iliyopitishwa
bungeni hapa nchini inatiliwa maanani. Kifungu cha kumi na mbili cha sheria hiyo
kinazuia uvutaji ua utumiaji wa bidhaa za tumbaku katika maeneo ya umma bali
vitendo hivyo bado vinashuhudiwa.
Aisha Mbaga

MbagaMambo vupi mpenzi msomaji wa safu hii ya mahaba? natumai kwa uwezo wa Mungu amekujaalia pumzi na umzima wa afya hapo ulipo unaungana nami katika mambo ya mahaba.
kama ilivyo ada ya mapenzi kuwa ni makubaliano kati ya wawili basihakuna haja ya kulazimishana katika kufanya mapenzi, hii ndiyo mada yetu ya leo.
Ukipendana na mtu kwa dhati, mtaheshimiana, hutafanya kitu chochote cha kumwuudhi au kumwuumiza, hutamlazimisha mwenzio kufanya kitu ambacho hapendi au hataki na wakati wote utataka kumfurahisha.
Kitu kimojawapo ambacho kitakutokea wakati unakua ni kuwa na mpenzi aliyekuingia moyoni au kupata mapenzi mazito.
Kumpenda mtu kunaweza kuwa kuzuri. Lakini mara nyingine kunaweza kukuchanganya akili hususan yanapojitokeza mambo ya kufanya mapenzi.
Wapo ambao wanafurahia mapenzi kwa kuwa wanapendana na wenzi wao lakini pia wapo wanaotamani kufa ama kujuta kuzaliwa kwa kuwana wapenzi ambao hawajatulia.
Ili kuepukana na majonzi hakikisha kuwa unayempenda naye anakupenda kisha hana papara ya ngono.
lama kwli anakupenda atakuvumilia nawe hakikisha kuwa unakuwa na msimamo wa kutofanya ngono hadi uwe tayari. ZIngatia mambo yafuatayo ikimpata mpenzi ili kuhakikisha kuwa unamsoma na kuupa moyo wako nafasi ya kufanya maamuzi.
LAZIMA MFANYE NGONOUkiwa na mpenzi unayempenda kwa dhati haina maana kwamba ni lazima mfanye nae mapenzi. Kitendo cha kufanya mapenzi kinatakiwa kiheshimiwe na kipewe hadhi yake kwa hivyo usikiendee kwa papara!
SUBIRI mpaka ukiwa tayari kimaumbile na kimawazo. Unaweza kuanza kufanya mapenzi ukiwa katika mapenzi ya dhati na ambayo unayaona yanaweza kumudu vishindo vyote.
USIKUBALI KUDANGANYWAUkiangalia filamu karibu zote zinazooneshwa siku hizi au ukizungumza na marafiki zako unafikiria kwamba kila mtu anafanya mapenzi wakati wote. Hii sio kweli kabisa! Watu wengi wanasubiri mpaka watakapokuwa watu wazima au wakishaolewa au kuoa.
EPUKA UONGO KATIKA MAPENZIUwapo utaweza kuwa mkweli kwa huyo unayemtarajia, ni wazi kuwa mnaweza kuelewana na ni rahisi sana kugundua tabua zake kwa kuwa wakati wote utakuwa mwazi kwake naye atajutahidu kuwa wazi na ukiona mpenzi wako ni mwongo basi hakufai tafuta njia ya kumfanya awe mkweli ama heri kukaa na kumtafuta mkweli kwani baadae unaweza kujutia mahusiano yako.
Unaweza kumpenda mpenzi wako na kuamua kutofanya naye mapenzi. Kama mpenzi wako anakupenda kwa dhati basi ataheshimu uamuzi wako na atakuwa mkweli kwako ikiwa ni pamoja na kukutunzia heshma yako.
pamoja na mila na desturi za Waafrika, mwanamke ameonekana kwa yeye ndiye anayelazimishwa kufanya ngono wakati hawako tayari, Hata wavulana wanalazimishwa kufanya mapenzi na wapenzi wao au hata marafiki zao. Sio vizuri kwa marafiki kuwashawishi wasichana au wavulana kufanya mapenzi wakati wao hawako tayari.
basi kwa leo tuoshie hapa ila usisahau kujiunga nami wiki ijayo,kwa waswaki na maoni wasiliana namoi kwa barua pepe yangu
Na Aisha Mbaga
Mambo vipi msomaji wangu wa safu ya Mahaba? Natumai kwa uwezo wa Mwenyezii Mungu umzima wa afya na waendelea vyema katika maandalizi ya mwanzo wa wiki.
natumai wiki iliyopita tuliangalia jinsi ya maandalizi ya wakati wa tendo la kujamiaana.
ninaimani nimeeleweka kwa wale waelewa. nawashukuru walionipigia simu kunipongeza na kunitaka ushauri.
Dada yangu salha wa Arusha ananiuliza jinsi ya kumlea Mwanaume, usijali, Salha kwani mwanaume mbele ya mwanamke ni sawa na mtoto mdopgo, waweza mliza upendavyo ila unachotakiwa ni kuwa mbunifu.
Leo tutazingumzia mambo muhimu katika kufikisha hisia zako. wapo baadhi ya watu hawawezi kumweleza mwanaume ukweli kuwa anampenda na matokeo anabaki akiumia bila kujua la kufanya. kwa upende wangu mimi sioni aibu endapo najikuta nipo penzini nakiwa mwazi.
jambo la kufanya kwa mwanaume umpendaye naye hajui kuwa unampenda, kwanza mwambie kama uwezo wa kufanya hivyo unao. wapo wanawake jasiri kwa kuweka mambo bayana na kujikuta wengine wanafanikiwa kutatua matatizo yao. baadhi ya watu wanaamini kuwa, kumweleza mwanaume ukweli kuwa unampenda ni utamaduni wa wazungu, mimi naamini kuwa katika hisia hakuna mzungu wala mwafrika.
Endpo huwezi kuweka mambo bayana tumia nwiki wako kuhakikisha kuwa unamteka mwanaume huyo kwa kumtega kwa kutumia njia tano muhimu
njia ya kwanza kuweza kumtega mwanaume ni mavazi.
unaweza kumtega mwanaume unayempenda kw akuimia mavazi, jaribu kuvaa vivazi vya kumvutia na kumfanya atahamaki kwa kukuwaza kila amapo kumbuka kivazi chako.
fanua jitikada za kujipitisha pitisha kila mara kwake huku ukiwa na vizawadi ambavyo vitamfanya awe rafuki yako na kumweleza wazi kuwa unapenda kuwa karibu naye hatakama hataki kuwa mpenzi wako.
jia ya pili, pendelea kutoka naye kila wakati ikiwa ni moja ya njia ya kumhamasisha na utokapo kuwa unamshangaza kwa kumpa zawadi ama kumwandalia chakila maakum ambacho unauhakika atakipenda na kitamvutia.
tumia sauti yako katika mazungumzo ili aweze kuvutika nayo kwani katika mahusiano, sauti inaweza kuchukua nafasi kumshawishi mwanaume na kujikuta akiiwaza na kuingia mtegoni.
pia hakikisha kuwa macho yako yanazungumza kwa kumtazama na kila ayaonapo ataona vimrlea vya mapenzi ndani ya mboni ya jicho lako na kujikuta kuwa anasogea karibu na wakati mwingine anaweza kukushangaza kwa kukuambia kuwa anakupenda japo hakuwa tayari kuwa na wewe.
wakati mwingine si lazima mwanaume aanza kupenda hata wanawake wanapenda na wananafasi ya kuonyesha mapenzi yao na kuhangaika hadi kufanikisha penzi lake kw ayule ampendae.
kwa leo tuishie hapo na usikose kuungana nami wiki ijayo. Alamsiki
kwa maoni na ushauri wasiliana nami kwa simu 0755690690.

Nawatakia watoto wenzngu wote maisha mema. na wale waishio katika mazingira magumu, mungu awasaidie waweze kuodokana na maisha hayo. nawaasa wamuombe mungu atawasaidia. wafadhili na matajiri wajitokeze kuwalea watoto hao ili wasijiingize katika makundi yasiyofaa.

Na Aisha Mbaga


UCHUMI wa MALAWI

UCHUMI-MALAWI:Kuwa ''Mwanafunzi Bora'' Kunaweza Kuwa Kubaya Kwako Pilirani Semu-Banda BLANTYRE, Aprili 17 (IPS) - Miaka mitano baada ya njaa ambapo zaidi ya watu 1,000 nchini Malawi walifariki dunia na wengine milioni 8 kati ya milioni 12 nchini humo walikabiliwa na njaa, kumbukumbu inayouma ya ushauri wa sera mbovu bado inaendelea. Shirika la Fedha Ulimwenguni (IMF) na Benki ya Dunia zililaumiwa kutokana na janga hilo ambalo liliipiga Malawi wakati wa njaa ya mwaka 2002. Shirika la kimataifa la kupigania haki za binadamu la Action Aid, kwa mfano, lilionyesha katika taarifa ya mwezi Oktoba 2002 kwamba IMF imeitaka serikali ya Malawi kuuza akiba ya nafaka kulipia deni lililokopwa na chombo kilichosajiliwa kisheria cha Wakala wa Hifadhi ya Chakula ya Taifa (NFRA). Ripoti hiyo iliyojulikana kama, ‘‘State of disaster: Causes, consequences and policy lessons from Malawi'', pia ilitaja Benki ya Dunia. Action Aid iliilaumu Benki ya Dunia kutokana na ‘‘kushinikiza'' Malawi kuuza mahindi kwa Kenya kulipia deni ambalo nchi hiyo ilikuwa ikidaiwa na Benki hiyo. Halafu Waziri Bakili Muluzi pia alitangaza wazi wazi kwamba Benki hiyo imekuwa ikishawishi serikali kuhifadhi fedha za kigeni kuliko nafaka. Nafaka, Benki hiyo ilisema, zinaweza kupoteza thamani. Hata hivyo, IMF na Benki ya Dunia zilikanusha shutuma hizo kwa kusema kwamba ‘‘zilikuwa washauri tu'' kwa serikali juu ya hifadhi yake ya nafaka. Walisema kwamba sababu za uhaba wa chakula nchini Malawi zilikuwa ngumu ikiwa ni pamoja na serikali kukaa kimya kutoa onyo la haraka, kupotosha habari katika masoko ya ndani na usimamiaji mbovu wa hifadhi ya chakula. Kufuatia shutuma hizo na kujibu shutuma hizo, mahusiano kati ya mashirika ya wafadhili na serikali yaliathirika. Hii ilisababisha kuchelewa kwa wafadhili kuchukua hatua wakati wa mgogoro wa chakula. Malawi imekuwa ikitegemea zaidi wafadhili kwa miongo minne. Fedha za wafadhili ambazo imeshazipata zinakaribia asilimia 40 ya bajeti ya taifa. Nchi hiyo imeshindwa kung’ata mkono ambao unailisha. Hivyo, pamoja na madai hayo ya sababu za mgogoro wa chakula, serikali ilikamilisha mageuzi ya kiuchumi katika kuzingatia masharti yaliyowekwa na Benki hiyo na IMF. Ikiwa kama zawadi, taasisi hizo zilifutia Malawi madeni yake mengi ya nje yanayofikia dola bilioni 2.97 Septemba 2006. Kumbukumbu za njaa hiyo na sababu yake bado zinaendelea kuwepo. Baadhi ya Wamalawi wanataka nchi hiyo kujinasua kutoka kwenye mtego wa taasisi hizo. Mkurugenzi wa Taasisi ya Utafiti wa Maendeleo ya Jamii ya Umoja wa Mataifa, Thandika Mkandawire, ambaye yeye mwenyewe ni raia wa Malawi, ni mmoja wa watu ambao anahofia mahusiano ya nchi hiyo na nchi wafadhili na taasisi za fedha za kimataifa. Anasema pamoja na Malawi kubatizwa jina la ‘‘mwanafunzi bora'' wa Benki hiyo na IMF kati ya mwaka 1980 na 1990, nchi hiyo inasimama kama mshtaka wa mahusiano ya misaada katika miongo mitatu iliyopita. Kati ya mwaka 1979 na 1999 Malawi ilichukua nafasi miongoni mwa kile IMF ilikipatia sifa ya ‘‘mtumiaji wa muda mrefu mno'' wa vifaa vyake. Taifa hilo lilikuwa na programu sita na IMF. Miaka 17 kati ya miaka 20 Malawi ilikuwa chini ya programu moja ya IMF hadi nyingine. ‘‘Katika nyaraka za IMF na Benki ya Dunia zilizokuwa zikifanyia tathmini matokeo ya sera za uchumi wa Afrika kati ya mwaka 1981 na 1998, Malawi iko juu zaidi katika orodha ya ‘warekebishaji bora' huku ikiwa imejitokeza mara saba, ikifuatiwa na Uganda na Kenya zikiwa za tano,'' anasema Mkandawire. Pamoja na ‘‘sifa hizo'', pato la taifa la Malawi lilishuka kutoka dola za Kimarekani 156 mwaka 1980 hadi dola 143 mwaka 1990. Hata ilipofika mwaka 2003 Malawi ilikuwa bado haijafikia kiwango cha pato la taifa cha mwaka 1979, kulingana na takwimu za Benki ya Dunia. Ripoti ya umaskini na kukosekana kwa utulivu iliyotolewa mwaka jana na serikali na Benki ya Dunia inaonyesha kwamba kumekuwepo na mafanikio madogo mno katika kupunguza umaskini na kukosekana kwa usawa. Mchanganyiko wa ushauri mbovu wa kisera na utawala wa kimabavu umezalisha miongo miwili iliyopotea kwa Malawi, anasema Mkandawire. Hakupendezewa na kukubali makosa kwa taasisi hizo au Mikakati ya Benki hiyo ya Kupunguza Umaskini. Ushauri wao umesababisha kuanguka kwa uwekezaji wa umma katika mtaji wa kimaumbile na kibinadamu, anasema. ‘‘Jambo ambalo hawaonekani kulitambua ni kwamba ongezeko la makosa limesababisha uchumi ambao haujarekebishwa vizuri na kushikiliwa katika mtego wa ukuaji mdogo,'' anasema Mkandawire. Mkandawire ana wasiwasi zaidi na jinsi ya kuingiliwa na nguvu za nje kunavyosababisha mataifa ya Afrika kupoteza uhuru wake. Mwaka 2002 IMF ilisitisha misaada yake ya kiuchumi kutokana na kile ambacho imekiita usimamizi mbovu wa uchumi chini ya rais wa zamani Muluzi. IMF ilirejesha programu yake baada ya utawala wa Bingu wa Mutharika, ambaye aliingia madarakani Mei mwaka 2004, kukubali kutekeleza sera zinazosimamiwa. Kwa njia hii rikodi zinazoeleweka za kutekeleza sera ziliundwa ili kuwarejesha wafadhili. Utekelezaji wa sera kwa mwaka wa kwanza ulishuhudia IMF na Benki kuizawadia Malawi kufuta asilimia 90 ya madeni yake ya kigeni. Msamaha wa madeni ulitafsiriwa kwamba Malawi ingeokoa dola za Kimarekani milioni 100 kama akiba ya kununulia bidhaa zake kutoka nje kwa mwaka kwani nchi hiyo iliendelea kuwa na mtaji ambao ungetakiwa kutumika katika kulipia madeni. Mkuu wa sera katika Action Aid Malawi, Collins Magalasi, pia hajaridhishwa na tabia ya mashirika wahisani. Anatoa mwito kwa nchi mfadhili wakuu wa Malawi, serikali ya Uingereza, kuongeza msaada wake wa kifedha ambao katika kipindi cha miaka mitano iliyopita ulifikia wastani wa pauni milioni 54.1 kwa mwaka, ambapo ni asilimia 0.0009253 tu ya pato la ndani la mwaka la Uingereza. Magalasi analaumu kuwa Wamalawi 70,000 wanafariki dunia kila mwaka kutokana na magonjwa yasiyozuilika. Kipato cha watu wote kikichanganywa hakilingani na ruzuku za kilimo ambayo Umoja wa Ulaya unatumia kwa wakulima wake. Wakati akielezea kuridhishwa kwake na misaada ya wafadhili ambayo nchi hiyo inapokea, Mutharika ametoa pia mwito wa ‘‘sera zinazobuniwa ndani ambazo zinapaswa kuungwa mkono na washirika wengine''. Katika mwaka wa fedha 2005/2006 serikali ilianza kutekeleza sera iliyoandaliwa ndani ya nchi iliyojulikana kama Mkakati wa Kukuza Uchumi na Maendeleo wa Malawi (MGDS), ambao utaendeshwa kwa kipindi cha miaka mitano. Mutharika anaona mkakati huo mpya kama chombo cha kuhamisha vipaumbele kwani ulibuniwa na Wamalawi. Wakati huo huo, unafanya kazi ya kurejesha nidhamu katika masuala ya fedha. Wafadhili wameunga mkono sera hiyo, kwa kukubali kuruhusu nafasi kwa sera zinazobuniwa na Wamalawi; na watu wa kawaida badala ya zile zinazobuniwa na wanauchumi na kuzimiliki. Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Haki ya Uchumi wa Malawi (Mejn), Andrew Kumbatira, anakubaliana kwamba MGDS ni sera iliyobuniwa ndani ya nchi ambapo mawazo ya ndani yamepewa nafasi kubwa mno. Anakubali kwamba ‘‘kuna sera zinazofanana na hizo katika mataifa mengine yanayoendela. Hii inaonyesha kwamba sera bado inaongozwa na wafadhili. Lakini jambo zuri kuhusu sera hii mpya ni kwamba mikutano ya ndani ya mashauriano ilikuwa mingi''.