Tuesday, August 30, 2011

Leo nimeona niongelee hii issue nzima ya serikali kuanzisha kampeni kabambe ya kuwakamata madaktari na kufunga mahospitali yanayo jihusisha na UTOAJI MIMBA…
Ofcouse sheria ya Tanzania hairuhusu watu kuchoropoa mimba. Ila hivi Serikali imefikiria the end result ya hii kampeni yao?
Niliona kwenye news ya TBC1 last week jinsi serikali ilivyofunga vituo kadhaa vya marie stoppes nchini kwasababu ya kukutwa wanajihusisha na utoaji mimba.
Basi juzi nilikuwa kwenye maongezi na watu kama wa 4 juu ya hili swala na wote tulikubaliana kwamba ni matatizo makubwa zaidi yatakayotokana na hii kampenzi. MORE BAD THAN GOOD WILL COME OUT OF THIS.
Unajua hata miji kama Dubai wanasheria inayosema kwamba mwanaume na mwanamke ambao hawajaona hawaruhusiwi kuishi pamoja, ila watu bado wanaishi pamoja na serikali imeamua kufumbia jicho hilo swala kwasababu wameona kuna mambo ambao ni ya muhimu zaidi kwa wao kuyafanya Dubai than kufatili nani analala na nani ili wawafunge jela.
Sasa mdau unajua kwamba sasa hivi kutokana na kwamba serikali inawasaka madaktari wanaotoa watu mimba biashara ya utoaji mimba imekuwa ni biashara yenye kuingiza pesa sana?
Unajua kwamba sasa bei ya kutoa mimba imepanda kutoa elfu 50,000 mpaka 600,000 WTF?????
Na jana kuna dada kaniambia kuna rafiki yake alipata matatizo hayo akaongea na daktari wa moja kati hizi hospitali kubwa pale Mikocheni akaambiwa aje na DOLA 400 tena kwa mimba isiozidi 2 months akaambiwa he is risking his career ndio maana bei imepanda sana. WTF????? Hivi hiyo dola 400 si ni laki 6 hiyo??
Hivi kuna wanatanzania wangapi wanaweza kuafford laki 6 kwenda kutoa mimba?? Sana sana watoto wa shule,hivi serikali inataka tuanze kuzaliana kama wachina? Au watoto waache shule? Na Serikali imeshapiga hesabu ni watoto wangapi ambao ni unwanted watakuwa wanazaliwa kila mwaka kutoka nah ii kampeni yao?je wameweka mikakatati gani kudeal na hili swala na hili ongezeko la watu litakalotokana nah ii kampeni yao?? Au mkakati wao ni kuongeza kodi kwa wananchi ili waweze kusupport hawa watoto ambao wengi wao wataishiwa kutupwa majajalani au kwenye vituo vya kulelea watoto??
Kilichonifnaya nikaja kuongea hii kitu leo ni kwamba kuna mtoto wa form 2 wa shule moja mjini hapa,ambae alikuwa na ujauzito akaenda Marie Stoppes wakamwambia wanaogopa kumtoa mimba na kama anataka apelike laki nne kwasababu mimba yake ilikuwa kubwa , huyo msichana baada ya kuona hizo pesa hawezi kuzipata alichokifanya ni kwamba alikwenda pharmacy akanunua chloroquine akamix na dawa zingine za miti shamba ili mimba itoke, kesho yake alikutwa na mama yake akiwa amefariki yeye pamoja na kichanga chake tumboni.
Mimi naona serikali ina mambo ya maana zaidi ya kufatilia,badala ya kuweka kampeni kabambe za kupambana na rushwa na ujinga mwingine nchini humu wanafatilia mambo ya utoaji mimba sasa wanamkomesha nani? Hawaoni kama wanawakomesha wanawake wan chi hii na kuwatajirisha madaktari????
Nasikia kuna daktari mmoja kaanza kutolea watu mimba nyumbani kwake anachaji laki 320,000 unaambiwa ukienda pale unakuta foleni . yani hakosei wateja kama 10 kwa siku embu niambie kwa siku anatengeneza shingi ngapi kwa kuchoropoa watu mimba tu???
Hivi kweli ndani ya mienzi miwili tu bei za kutoa mimba zimepanda kutoka kati ya 30,000 na 50,000 mpaka kufikia laki 350,000 mpaka 600,000. its absurd.

No comments:

Post a Comment